RUGE ALIKUWA MSTARI WA MBELE KUWASAIDIA VIJANA-MAJALIWA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 27 February 2019

RUGE ALIKUWA MSTARI WA MBELE KUWASAIDIA VIJANA-MAJALIWA

Waziri Mkuu, Kassim  Majaliwa  na mkewe Mary (wa pili kulia) wakimfariji mama Mzazi wa marehemu Ruge Mutahaba, Christiana Mutahaba wakati  walipokwenda nyumbani kwao  marehemu, Mikocheni jijini Dar es salaam, kutoa pole kwa familia ,  Februari 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na baba mzazi wa marehemu Ruge Mutahaba wakati alipokwanda nyumbani kwao marehemu, Mikocheni jijini Dar es salaam  kutoa pole kwa familia, Februari 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu, Kassim  Majaliwa  na mkewe Mary (wa pili kulia) wakimfariji mama Mzazi wa marehemu Ruge Mutahaba, Christiana Mutahaba wakati  walipokwenda nyumbani kwao  marehemu, Mikocheni jijini Dar es salaam, kutoa pole kwa familia ,  Februari 27, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Taifa limepoteza kijana aliyekuwa msatari wa mbele kuwahamasisha vijana wajitambue wawe wazalendo kwa nchi yao na watambue fursa za maendeleo zilizopo na wasiwe walalamikaji.

Ameyasema hayo Februari 27, alipokwenda kuhani msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba kwa niaba ya Serikali, nyumbani kwa wazazi wa marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu amesema vijana nchini walikuwa na kiongozi aliyekuwa akiwaongoza kwa kuwafungua kimawazo na kuwaonesha fursa mbalimbali zitakazowawezesha kuwakwamua kifikra na kiuchumi ili waweze kujitegemea.

Waziri Mkuu amesema msiba huo ni wa wote kwani marehemu amefanya kazi kubwa ya kushirikiana na Serikali kuhamasisha vijana kujitambua na kutambua fursa zilizpo na kuzifanyia kazi. “Ruge ametoa mchango mkubwa kwa Taifa

Amesema marehemu Ruge katika kipindi cha uhai wake amefanya kazi kubwa kwa upande wa Serikali, kuanzia awamu ya nne hadi ya tano hususani katika suala la kuhamasisha vijana kujikwamua na kutokuwa wategemezi.

Pia, Waziri Mkuu amesema historia yake inaeleza namna alivyozunguka nchi nzima na kukutana na makundi ya vijana mbalimbali na kuwaelimisha namna ya kutambua fursa zilizopo nchini huku akiwahamasisha wawe wazalendo.

"Marehemu alikuwa akitoa hadi fedha zake binafsi kwa ajili ya kuwawezesha vijana hasa wale ambao hawakuwa na uwezo wa kiuchumi ili nao washiriki katika shughuli mbalimbali za ujasiriamali na hatimaye waondokane na utegemezi.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ametoa wito kwa wazazi, watoto wa marehemu pamoja na wananchi kwa ujumla waendelee kuwa na subira na watulivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao. 

No comments:

Post a Comment