![]() |
| Sehemu ya viongozi wa Taasisi ya Afya na Tumaini Endelevu (ATE), wakipata picha ya pamoja mara baada ya kutoa elimu kuhusu masuala ya hedhi salama na umuhimu wa elimu hiyo kwa wasichana. |
![]() |
| Mwenyekiti wa Taasisi ya Afya na Tumaini Endelevu (ATE), Lilian Lema (kulia) akigawa msaada wa taulo za kike kwa wanafunzi hao, mara baada ya kutoa elimu ya hedhi salama shuleni hapo. |
Na Mwandishi
Wetu, Dar
TAASISI ya
Afya na Tumaini Endelevu (ATE) imetoa elimu ya afya ya hedhi kwa wasichana wa
Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko ya jijini Dar es Salaam, pamoja na msaada wa
pedi hizo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya hedhi salama duniani.
Akizungumza
katika tukio hilo lililoenda pamoja na utoaji wa msaada wa pedi hizo kwa kundi
hilo la wasichana wenye mahitaji maalum, Mwenyekiti wa ATE, Bi. Lilian Lema amesema
wametoa elimu ya afya ya hedhi kwa wasichana hao ili iweze kuwasaidia.
“Leo tunatoa
elimu kuhusu hedhi salama, usafi wa mwili wa mwanamke, na tunagawa pedi pamoja
na kuhamasisha jamii kuwalinda watoto kuanzia ngazi ya familia na vitendo vyote
vya unyanyasaji wa kijinsia,” alisema Bi. Lema katika ziara hiyo.
Alisema
wameguswa kusaidia kundi hilo la wasichana wenye mahitaji maalumu kwa sababu
mara nyingi hukumbana na changamoto katika kupata taarifa sahihi, vifaa vya
hedhi salama, na mazingira yanayowajali.
Taarifa
zaidi zinabainisha baadhi ya wasichana hujikuta wakikosa masomo kwa siku tatu
hadi saba kila mwezi wanapokuwa kwenye hedhi kwa sababu ya kukosa ‘pedi’.
Wasichana
hao hulazimika kubaki nyumbani wakihofia kuchafuka na kuaibika mbele za watu,
huku wakijikuta wakikosa fursa ya kushiriki masomo na wenzao kwa kipindi hicho.
Bi. Lema alifafanua zaidi kuwa, upatikanaji wa uhakika wa pedi kwa wanafunzi wa kike wakiwemo wa shule za msingi na sekondari nchini utaimarisha elimu ya mtoto wa kike kiujumla.
"Mtoto
wa kike anapokuwa na uhakika wa kupata vifaa vya kujihifadhi anapokuwa katika
siku zake inampa amani ya kujifunza na kuzingatia masomo yake bila ya kuwa na
wasiwasi wa kuchafuka,"alisema.
Naye, Makamu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Ajrath Kashakara amewaomba wadau anuai kuendelea kutoa elimu kuhusu masuala ya hedhi salama na umuhimu wa elimu ili kuendelea kubadilisha maisha ya wasichana na jamii ya kitanzania.



.jpg)




No comments:
Post a Comment