MFUKO WA KUSAIDIA ELIMU WAPIGA HODI ITIGI - THE HABARII

THE HABARII

HABARI | MATUKIO | MICHEZO.


ASAS GROUP

Habari Mpya


Friday, 14 August 2026

MFUKO WA KUSAIDIA ELIMU WAPIGA HODI ITIGI

p>
Mhe. Ally Minja Diwani wa Kata ya Itigi Mjini, ambaye ameandika andiko la kuanzisha Mfuko wa Elimu katika Wilaya ya Itigi mkoani Singida akizungumzia faida ya mfuko huo Agosti 12, 2026. Kulia ni Diwani wa Kata ya Ipande, Kedmon Mpondo.

MFUKO wa Kusaidia Elimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Itigi mkoani Singida unatarajia kuanzishwa baada ya Diwani wa Kata ya Itigi Mjini Ally Minja kuandika andiko na kulipeleka kwa madiwani na kupokelewa kwa mikono miwili.

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani lililoketi Agosti 12, 2026 kwa lengo la kupokea, kupitia na kujadili taarifa za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo (ikiwemo miundombinu, afya, elimu na maji) kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Itigi, Mhe. William Lupaa alisema wazo hilo limepokelewa kwa mikono miwili na  Madiwani.

“ Wazo hili kupitia andiko la Mhe. Ally Minja Diwani wa Kata ya Itigi Mjini ni zuri na tumelipokea kwa mikono miwili lakini tumelipeleka kwenye Kamati ya Elimu na Afya ili likajadiliwe na kuona hatua nyingine zitakazo fuata,” alisema Lupaa.

Akizungumzia manufaa ya mfuko huo Mhe Minja alisema suluhisho la pamoja aliloliona hadi kufikia tafakari hiyo ni kuiomba Halmashari ya Wilaya ya Itigi kuanzisha Mfuko wa Elimu kwa ajili ya kukusanya rasilimali fedha kutoka maeneo mbalimbali.

“Fedha zitakazopatikana zitawasaidia watoto na kizazi chetu kiweze kupata elimu,” alisema Minja.

Minja alisema ikumbukwe kwamba kipaumbele cha elimu ni kikubwa kuliko vingine vyote na ndiyo urithi mkubwa ambao ni miongoni na ule watakao achiwa.

  Akielzea namna ya kupata fedha hizo ni pamoja na kuanzisha uhamasishaji wa upatikanaji wa fedha ya kusomesha watoto wetu na njia bora nyingine za kupata fedha hizo.

Akitolea mfano mwingine alisema “Agosti 11 katika halmashauri hiyo ulifanyika mnada wa kuuza kilo milioni 2.5 za dengu ambapo kama tukiwaomba wakulima kupitia vyama vyao  angalau shilingi 10 tu kwenye kila kilo ambayo inaweza kuonekana haina kazi  lakini kwa mnada huo uliofanyika wangeweza kupata shilingi milioni 25.

“Kwa mnada wa jana tu tunge weza kupa kiasi hicho cha fedha ambazo zingeingia kwenye mfuko huo na mpaka minada mingine ije imalize msimu ingekuwa tumepata shilingi ngapi,” alihoji Minja.

Aidha, Minja alisema hiyo ni kwa zao la ndengu je wakienda kwenye zao la pamba ambalo linauzwa kwa ushirika ambayo inalimwa kwenye vijiji vya Kitaraka, Lyandole na kata nyinge hapo hawajaenda kwenye zao la tumbaku na kupata michango kutoka taasisi mbalimbali na Asasi nyingine kuchangia elimu.

Minja aliongeza kuwa hilo wazo linaweza kuonekana la kawaida kwa sasa kwa sababu baadhi ya watu wamezoea kuweka ubinafsi mbele lakini shida ya mtoto kukosa fedha za kumuendeleza kusoma shule linaikumba kila nyumba.

Alisema hali hiyo  ni kama ilivyo kwa maradhi na katika ukoo ambao haujawahi kukumbwa na changamoto ya mtoto kushindwa kuendelea na masomo kwa kukosa rasilimali fedha hivyo halmashauri hiyo ikianzisha mfuko huo itaweza kusaidia watoto kwa mamia kuweza kuendelea na masomo ambao utakuwa msaada mkubwa sana.

Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Itigi, Mhe. William Lupaa (katikati) akiongoza Baraza la Madiwani lililoketi Agosti 12, 2026 mkoani Singida. Kutoka Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ayubu Kambi, Kaimu Katibu Tawala wa wilaya hiyo Charles Magesa na Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya yaa Manyoni na Itigi, Maimuna Makunguni.

Madiwani wakiwa kwenye kikao hicho.

Waratibu wa vikao wa Halmashauri hiyo (CC), wakiwa kazini. Kushoto ni Juliana  Jephata Kaaya na Makandaiga Chacha Magabe wakishiriki baraza hilo.

Habari hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990. 

No comments:

Post a Comment