Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea Banda la Wizara ya Viwanda na Biashara katika Maonesho ya Wakulima Nanenane Kitaifa 2026 yanayofanyika Viwanja vya Dk. John Malecela Jijini Dodoma Agosti 7, 2026.
SERIKALI
inawajibu wa kumtengenezea mazingira rafiki Mtanzania ili kumurahisishia
shughuli zake za kiuchumi.
Hayo
yamebainishwa na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dennis Londo, wakati
akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea Banda la Wizara ya Viwanda na
Biashara katika Maonesho ya Wakulima Nanenane Kitaifa 2026 yanayofanyika Viwanja vya
Dk. John Malecela Jijini Dodoma Agosti 7, 2026.
“ Kila
Mtanzania anapaswa kutengenezewa mazingira rafiki awe mkulima, mfugaji na
mvuvi,” alisema Mhe. Londo.
Mhe. Londo
aliongeza kusema kuwa mwananchi anapopunguziwa gharama hizo anakuwa na uhakika
wa kuzalisha kwa tija na kuwa na uhakika wa kuwa na akiba ya chakula cha kutosha.
Aidha, Naibu
Waziri Londo alisema Serikali inachokifanya ni kujenga barabara, vivuko na
madaraja ili kumuwezesha mkulima kutoka mashambani kwenda kwenye masoko na viwandani.
Alisema
Serikali hivi sasa inaendelea kusambaza umeme kupitia Wakala wa Umeme Vijijini
(REA) katika vijiji na vitongoji vyote
ili kumpunguzia gharama mwananchi za uzalishaji.
Habari hii imeandikwa na Dotto Mwaibale namba ya simu 0754362990.

No comments:
Post a Comment