DKT. NCHEMBA AISHUKURU BENKI YA UBA KWA USHIRIKIANO WAO KATIKA MIRADI YA MAENDELEO - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Tuesday 8 October 2024

DKT. NCHEMBA AISHUKURU BENKI YA UBA KWA USHIRIKIANO WAO KATIKA MIRADI YA MAENDELEO

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa United Bank of Africa (UBA), Bw. Gbenga Makinde, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha Jijini Dar es Salaam, ambapo ameishukuru Benki hiyo kwa kuwa tayari kuendelea kushirikiana na Serikali katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (Katikati), alipokutana na Mkurugenzi Mtendaji wa United Bank of Africa (UBA), Bw. Gbenga Makinde (Kulia), katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha Jijini Dar es Salaam, ambapo ameishukuru Benki hiyo kwa kuwa tayari kushirikiana na Serikali katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere. Kushoto ni Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Madeni, Bw. Japhet Justine.

Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam

WAZIRI wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), ameishukuru United Bank of Africa (UBA), kwa kuwa tayari kushirikiana na Serikali katika kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo.

Dkt. Nchemba, ametoa shukrani hizo alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa United Bank of Africa (UBA), Bw. Gbenga Makinde, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha Jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa Serikali inatekeleza miradi mingi ya kimkakati kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake na kuialika Benki hiyo kuwekeza katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo reli na umeme. 

Kwa upande wake, Bw. Makinde, ameeleza kuwa Benki yake imekuwa ikishirikiana na Tanzania katika kutekeleza baadhi ya miradi yake ya kimkakati ikiwemo Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere, kwa kuwawezesha kifedha wakandarasi wanaojenga mradi huo na kwamba hivi sasa Benki hiyo iko tayari kushirikiana moja kwa moja na Serikali kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi husika.

UBA ni Taasisi ya fedha ambayo iko nchini kwa miaka 15 na ina matawi zaidi ya 20 katika nchi za Afrika, na baadhi ya nchi za ulaya na Marekani.

No comments:

Post a Comment