KAWASO YAPATA UONGOZI MPYA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 6 May 2024

KAWASO YAPATA UONGOZI MPYA




VIONGOZI wa Chama cha Wamachinga Kariakoo (KAWASO), wamesema wataendelea kupigania changamoto za wamachinga wa Kariakoo na Tanzania kwa ujumla.

Hayo yameelezwa  na Mweneyekiti wa Kawaso, Stephen Lusinde alipofanya mahojiano  makao makuu ya Kawaso Kariakoo Dar es Salaam.

“Ninamshukuru Mungu mimi binafsi na kwa niaba ya viongozi wenzangu, wajumbe, na wanachama wote walioturudisha madarakani na hata ambao hawakutuchagua tutawatumikia pasipo ubaguzi wowote kwani wito wetu ni kuwatumikia wamachanga” alisema Lusinde

Aidha Lusinde amewataka wamachinga kuendelea kufanya kazi kwa umoja na ushirikiano na wasisite kuona uongozi pale zinapotokea changamoto kwakuwa wapo kwa ajili ya kuwatumikia.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kawaso, Yusuphu Namoto amesema haikuwa rahisi kushinda uchaguzi huo kutokanana na mizengwe ya hapa na pale lakini walimuachia Mungu ili achukuwe nafasi yake katika jambo hilo adhimu na muhimu katika Maisha yao kama wafanyabiashara.

“Ifahamike kwamba tokea kuanzishwa kwa Kawaso tokea 2017 hakujawahi kufanyika uchaguzi wowote na huu ndiyo uchaguzi wa kwanza kufanyika na wanamshukuru Mungu na wapiga kura kwa kuwaamini na kuwarejesha madarakani” alisema Namoto

Akizungumzia siri ya ushindi wao alisema ni kujituma katika katika kuwatumikia wamachinga hususani utatuzi wa changamoto zinazowakabili kadri ya uwezo wao.

Uchaguzi huo ulifanyika April 26, 2024, ambapo Stephen Lusinde amerejeshwa katika nafasi yake ya Uenyekiti, Namoto akiwa Makamu Mwenyekit, na Katibu ni Borno Nanyimbura, Naibu Katibu ni Sabiti Maloua, Mhazini Ally Haji, Agostino Choga.

Wengene ni wajumbe wa kamati tendaji, kamati ya Nidhamu ni Hassan Chande, Ndugura Majegeja na Dickson Fedirick,Kamati ya Fedha ikiongozwa na Umi Chakati, Johanitha Mtelan na Jabiri Ndegeja. Kamati nyingine ni kamati tendaji.

No comments:

Post a Comment