MFUMO WA BREAK KWENYE GARI (ABS) - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday 20 November 2021

MFUMO WA BREAK KWENYE GARI (ABS)

Sehemu ya mfumo wa breki kwenye gari.

Anti lock braking system or anti-skid braking system (ABS). Huu ni mfumo wa umeme wa usalama unaoruhusu tairi katika kujidhibiti kimpangilio wa mtetemo iwapo barabarani sawia na tukio la dereva anapofunga brake na kusababisha gurudumu kujifunga na kupunguza mwendo na kuepusha gari kukosa muelekeo.

Kwa kawaida unapokanyaga brake.. Momentum/ nguvu ya uzito na mwendo hukimbilia  kwenye matairi ya mbele. 

Karibu asilimia 60 huenda mbele na 40% kuwa nyuma. 

Hivyo matairi ya mbele huwa na brake zenye uwezo zaidi kuliko za nyuma. 

Mara nyingi unaweza kuona kuwa wheel cylinders za mbele ni kubwa kuliko za nyuma au mbele ni disk lakini nyuma ni brake shoes. 

Ushikaji  wa brake za mbele kuwa tofauti na za nyuma hauna  madhara. 

Kuna madhara makubwa yanaweza kutokea endapo brake za kushoto zitashika tofauti na za kulia. 

Hapo tegemea shida.

Mambo yanayoweza  kusababisha brake za kushoto kushika zaidi au kidogo kuliko kulia ni mengi. 

Baadhi ni kama:

(1) endapo upande mmoja paipu ya mafuta ya brake imepasuka  (2) tairi la upande moja rubber za wheel cylinders zinavuja

(3)  tairi moja limepita  kwenye maji /dimbwi jingine hapana

(4)  tairi moja limepita  mahali pana utelezi  kama pana mafuta au mchanga nk 

Ushikaji wa brake ukitofautiana kati ya tairi la kulia na kushoto ni tatizo kwa kuwa lile  lililo shika brake litakuwa linasota (skidding) wakati lisiloshika brake litaendelea kutembea. 

Kitendo  cha tairi moja kushika  brake lingine kutoshika  kinaweza kuleta madhara makubwa. 

Kwani gari litavuta  upande ulio shika brake na kama uko speed kubwa waweza kupinduka  kabisa!! 

Kazi ya ABS ni nini sasa?

Ni kuzuia  skidding ndiyo maana ABS inaitwa Anti-Skidding-Brake System 

System hii ni ya kielectronic na kazi yake ni kuhakikisha kuwa tairi zote kulia na kushoto zinashika  brake sawia. 

Na hufanya hivi kwa kusimamisha ushikaji wa brake ile inayohusika zaidi ya mwenzake!!  

Hatimaye kuhakikisha kuwa hakuna skidding au tairi moja kushika  zaidi ya jingine.

Natumai mmenielewa. 

RSA Tanzania

Usalama barabarani ni jukumu letu sote

No comments:

Post a Comment