TTCL YAFUTURISHA WATOTO YATIMA NA WAZEE ZANZIBAR - THE HABARII
.com/img/a/
ASAS GROUP
.com/img/a/

Thursday, 27 March 2025

demo-image

TTCL YAFUTURISHA WATOTO YATIMA NA WAZEE ZANZIBAR

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.15_1d9a44f6
Sehemu ya waalikwa wakifuturu katika futari iliyoandaliwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kufanyika Kituo cha Wazee cha Sebuleni, jana jijini Zanzibar ikiwa ni sehemu ya ibada na kushirikiana na jamii kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.


WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.17_df0da256
Sehemu ya waalikwa wakifuturu katika futari iliyoandaliwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kufanyika Kituo cha Wazee cha Sebuleni, jana jijini Zanzibar ikiwa ni sehemu ya ibada na kushirikiana na jamii kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.


WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.18_bcfd4f49
Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, akiwaongoza waalikwa wengine katika futari iliyoandaliwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kwenye Kituo cha Wazee cha Sebuleni, jana jijini Zanzibar ikiwa ni sehemu ya ibada na kushirikiana na jamii kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.19_79dbf231

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.19_f330ab71

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.20_a20fe312

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.21_2bdd8471

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.21_6cb32dcb

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.21_e5c24303

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.22_30015b75
Meneja wa TTCL Zanzibar, Bw. Hilaly Mwinyi akizungumza katika futari iliyoandaliwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kufanyika Kituo cha Wazee cha Sebuleni, jana jijini Zanzibar ikiwa ni sehemu ya ibada na kushirikiana na jamii kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.23_37aa76ef
Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, akizungumza katika futari iliyoandaliwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na kufanyika Kituo cha Wazee cha Sebuleni, jana jijini Zanzibar ikiwa ni sehemu ya ibada na kushirikiana na jamii kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.24_fee5c207
Meneja wa TTCL Zanzibar, Bw. Hilaly Mwinyi (wa pili kushoto), pamoja na Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi (wa tatu kushoto) wakikabidhi sehemu ya msaada wa mahitaji mbalimbali uliotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa Kituo cha yatima cha Mazizini.

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.24_ffba1b1a

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.25_272197b7

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limefuturisha Watoto wa Kituo cha Yatima Mazizini pamoja na Wazee wa Kituo cha Sebuleni, vyote vya jijini Zanzibar ikiwa ni sehemu ya ibada na kushirikiana na jamii kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Ibada ya futari hiyo imefanyika jana kwenye Ukumbi wa Kituo cha Wazee cha Sebuleni Zanzibar, iliyokwenda sambamba na kukabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali kwa watoto yatima wa kituo hicho cha Mazizini.

Akizungumza katika hafla hiyo, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, ameipongeza TTCL kwa kuandaa futari na kutoa msaada kwa watoto yatima na wazee.

"Michango yenu leo inaonesha mshikamano wa TTCL na jamii pamoja na kujali mahitaji ya wasiojiweza," alissisitiza Sheikh Wadi.

Naye, Meneja wa TTCL Zanzibar, Bw. Hilaly Mwinyi alisema TTCL itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo ya mawasiliano nchini Tanzania, kwani inaamini kuwa ujenzi wa Tanzania ya kidijitali ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi kijamii na kielimu.

Alibainisha kuwa Mwezi wa Ramadhani ni wakati wa ibada, toba, na kujitakasa, kushirikiana, kusaidiana, na kuwajali wenzetu wenye uhitaji zaidi ndio maana tumeungana kwa jambo hili.

Liongeza kuwa kwa kutambua umuhimu wa ependo wa mshikamano huu ndio maana TTCL imeona ni jambo la busara leo kushirikiana na jamii kwa kuandaa futari kwa wazee na watoto hawa hapa mjini Zanzibar.

Aidha amesema TTCL itaendelea kushirikiana na jamii kwa njia mbalimbali ili kuhakikisha kuwa michango ya shirika inawafikia wale wanaohitaji zaidi.

”Tunajitahidi sio tu katika kuimarisha mawasiliano na huduma za kidijitali nchini, bali pia katika kujenga jamii yenye mshikamano, huruma, na maendeleo endelevu” amesema Bw. Mwinyi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Ustawi wa Jamii na Wazee, Bw. Hassan Ibrahim Suleiman, alisifu TTCL kwa kuendelea kuwasaidia wazee na watoto yatima. "Hii sio mara yako ya kwanza kutuonyesha wema; mnakuwa mfano wa kampuni nyingine," alisema. 

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.15_c9f9d3aa

WhatsApp%20Image%202025-03-27%20at%2011.55.18_988a008d
Halotel+Mpango+Mzima

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *