DKT. NCHEMBA AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI BENKI YA NCBA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 8 May 2024

DKT. NCHEMBA AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI BENKI YA NCBA

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kushoto) akizungumza jambo wakati wa mkutano na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NCBA Tanzania Bw. Claver Serumaga, ulioangazia ushirikiano wa maendeleo, katika Ofisi ya Waziri wa Fedha Treasure Square, jijini Dodoma.

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NCBA Tanzania Bw. Claver Serumaga, akieleza utayari wa Benki yake wa kuongeza ushirikiano katika nyanja za maendeleo wakati wa mkutano kati yake na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) uliofanyika katika Ofisi ya Waziri wa Fedha Treasure Square, jijini Dodoma.


Kamishna wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Dkt. Charles Mwamwaja (kulia), akifafanua jambo wakati wa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NCBA Tanzania Bw. Claver Serumaga (hawapo pichani), ulioangazia ushirikiano wa maendeleo, katika Ofisi ya Waziri wa Fedha Treasure Square, jijini Dodoma.



Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kulia) wakiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NCBA Tanzania Bw. Claver Serumaga, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Benki hiyo na Serikali katika kuchangia maendeleo, katika Ofisi ya Waziri wa Fedha Treasure Square, jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment