Waziri wa Ujenzi, Innocent
Bashungwa akifafanua jambo kwa Mkurugenzi wa Matengenezo kutoka Wakala ya
Barabara (TANROADS), Dkt. Christina Kayoza na Meneja wa TANROADS Mkoa wa Pwani,
Eng. Baraka Mwambage wakati akikagua urejeshaji wa miundombinu ya barabara kuu
ya Lindi – Dar es Salaam eneo la Somanga, tarehe 07 Mei, 2024 Mkoani Lindi.
Mkurugenzi wa
Matengenezo kutoka Wakala ya Barabara (TANROADS), Dkt. Christina Kayoza akitoa
taaarifa kwa Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa kuhusu hatua zilizofikiwa za
urejeshaji wa miundombinu ya barabara kuu ya Lindi – Dar es Salaam eneo la
Somanga ambalo lilikatika kutokana na mvua zilizonyesha na kuambatana na
Kimbunga Hidaya Mkoani Lindi. Kulia ni Meneja wa TANROADS Mkoa wa Pwani, Eng.
Baraka Mwambage. |
Waziri wa Ujenzi
Innocent Bashungwa amesema hatasita kubadilisha timu ya Wataalam na Mkandarasi
wanaoendelea na kazi ya kurejesha mawasiliano ya barabara ya Dar es Salaam-
Lindi katika eneo la Nangurukuru kutokana na kasi ndogo ya kazi na usimamizi.
Bashungwa ameonesha
hali hiyo ya kutoridhishwa na usimamizi na kasi ya urejeshaji wa mawasiliano
katika eneo hilo na kumtaka Mtaalamu na Mkandarasi kuongeza kasi ili wamalize
zoezi ndani ya muda uliotolewa.
"Mimi naweza
kufukuza timu yote, bora niwaambie watanzania timu hii imefeli na niagize
nyingine ambayo inaweza ikaja kufanya kazi, hatuwezi kwenda hivi", amesema
Bashungwa.
Aidha, Bashungwa
amemuagiza Mkurugenzi wa Matengenezo ya Barabara - TANROADS kutafuta na kuongeza magari ya kubeba
mawe na vifusi pamoja na mitambo ili kazi ifanyilke usiku na mchana bila
kusimama.
Kwa upande wake,
Mkurugenzi wa Matengenezo kutoka Wakala ya Barabara (TANROADS), Dkt. Christina
Kayoza ameahidi kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika eneo la
Nangurukuru katika upande wa usimamizi na pia ameeleza kuwa amekwishafanya
maandalizi ya upatikanaji wa mawe na mitambo ili yaweze kufika katika eneo hilo
na kuongeza kasi ya urejeshaji wa miundombinu ya barabara yaliyokatika.
No comments:
Post a Comment