SABABU YA WANAUME KUKWEPA KWENDA NA WENZA WAO KLINIKI YATAJWA, ILEKANILO... - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday 5 February 2023

SABABU YA WANAUME KUKWEPA KWENDA NA WENZA WAO KLINIKI YATAJWA, ILEKANILO...

 

 John Maongezi Mratibu wa Mradi wa Afya ya Jamii wilaya ya Kahama kupitia shirika la Americares akizungumza na makundi mbalimbali ikiwemo Vijana, Wazee na Viongozi katika kijiji cha Ilekanilo Kata ya Kasungamile Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza ikiwa ni utekekelezaji wa mafunzo ya Tathmini   Shirikishi ya Kijamii (Community Score Card) ambayo ni moja ya Afua ya Ushirikishaji Jamii  yanayoratibiwa na Wizara ya Afya, Idara ya Kinga, Elimu ya Afya kwa Umma, Mpango wa Huduma za Afya ya Jamii kwa kushirikiana na AMERICARES Kupitia Mradi wa  USAID Uzazi Staha.

Na Faustine Gimu, Sengerema-Mwanza

JAMII imetakiwa kubadili tabia na kuona kuwa wanawake kuambatana na wenza wao vituo vya kutolea huduma za Afya ni jambo la kawaida.

Hayo yameibainishwa katika kijiji cha Ilekanilo, Kata ya Kasungamile Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza baada ya timu iliyonufaika na Mafunzo ya Tathmini Shirikishi ya Kijamii (Community Score Card) ambayo ni moja ya Afua ya Ushirikishaji Jamii yanayoratibiwa na Wizara ya Afya, Idara ya Kinga, Elimu ya Afya kwa Umma, Mpango wa Huduma za Afya ya Jamii kwa kushirikiana na AMERICARES Kupitia Mradi wa USAID Uzazi Staha kufika katika kijiji hicho na kushirikisha jamii namna huduma za afya zinavyotolewa.

Akizungumza katika kijiji cha Ilekanilo ikiwa ni utekelezaji wa Mafunzo ya Tathmini Shirikishi ya Kijamii (Community Score Card) kupitia mpango wa Huduma za Afya ya Jamii, Mratibu wa Uhamasishaji na Uelimishaji Elimu ya Afya ngazi ya Jamii (DCBHPco) Wilaya ya Sengerema Rachel Ntogwisangu amesema asilimia kubwa wanaume wa Sengerema wamekuwa wakikwepa kuambatana na wake zao vituo vya kutolea huduma za afya hasa kipindi cha ujauzito wakikwepa kuchekwa na jamii iwapo hawajawatunza hivyo amesema ni muhimu wenzi wote wawili kubadili tabia na kuongozana kwenda kliniki.

“Mjamzito ni muhimu sana kwenda kupata huduma za afya akiambatana na mmewe, hii itasaidia kushauriana kwa pamoja namna ya kupanga uzazi na malezi sahihi na ushauri wa watalaam wa afya kwa pamoja hata kama kuna viashiria vya maambukizi upataji wa huduma sahihi kwa wote ni rahisi “amesema

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Kasungamile Wilayani Sengerema Mkoani Mwanza Godfrey Joseph ambaye alikuwa mwenyekiti katika mkutano huo shirikishi kwa jamii kuhusu huduma za Afya ameishukuru Wizara ya Afya kwa kuja na Mpango huo Shirikishi hali itakayosaidia wananchi kubadili tabia na kuwa na matokeo chanya.

“Tumekuja kupata elimu ya pamoja hii itasaidia baada ya siku chache mambo yatakwenda vizuri,tunaishukuru sana Wizara ya Afya kwa kuja na Mpango shirikishi na tuendelee kushirikiana kwa ujumla katika uboreshaji wa huduma na tumeshirikishwa kwa kuulizwa maswali je, tunapokeaji huduma na si kwa ugomvi ni namna nzuri tu ya kurekebisha kasoro ndogondogo ili sote twende pamoja” amesema.

 Afisa Program huduma za afya ngazi ya jamii, Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma, Idara ya Kinga, Wizara ya Afya Orsolina Tolage amesema Wizara ya Afya kupitia Mpango wa Huduma za Afya ya Jamii itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo katika kuhakikisha jamii inakuwa na mabadiliko chanya katika masuala ya Afya na kuwataka vijana kuwa mstari wa mbele kwa masuala hayo.

 "'Jukumu la Wizara ya Afya kuendelea kutoa Miongozo, kusimamia na kufanya ufuatiliaji" amesema.

 Mratibu wa Huduma za Afya katika jamii kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa [OR-TAMISEMI] Martha Mariki akisema wataendelea kusimamia sera katika kuhakikisha huduma za Afya zinaimarishwa ngazi ya Jamii

 

 

Mratibu wa Uhusiano Jamii na Mabadiliko ya Tabia kutoka  Americares Mussa Lunyonga amesema hatua hiyo ya Mafunzo ya Tathmini Shirikishi ya Kijamii (Community Score Card) kupitia Wizara ya Afya, Mpango wa Huduma za Afya ya Jamii kwa kushirikiana na AMERICARES  na TAMISEMI imekuwa na chachu kubwa kwa wananchi kueleza namna wanavyopokea huduma za afya na kurahisisha namna ya kuweka mikakati ya pamoja katika uboreshaji.

Nao baadhi ya Wananchi wa kijiji cha Ilekanilo akiwemo Bugumbi Mwarabu, Jackson Mletwa, Yubi Busenga pamoja na Lucas Petrol wamesema Mafunzo shirikishi yamesaidia kuwabadili tabia hususan Elimu ya Afya ya Uzazi huku wakizungumzia chanzo kinachosabisha vijana wa kike kwenda vituo vya kutolea huduma za Adfya peke yao bila wenzi.

“Unakuta kijana wa kike amekutana na waume wanne watano, inapofika muda anashindwa hiyo mimba anampa nani hivyo hivyo kijana wa kiume naye unakuta ana wasichana sita matokeo yake ni kukataa mimba, matokeo yake anafika kwenye zahanati akiwa peke yake,”amesema Bugumbi.

Katika Mafunzo shirikishi haya kwa upande wangu binafsi naishukuru sana Wizara ya Afya kuanzia leo najua uzazi wa Mpango ni nini kwa hiyo mimi kama kijana nimeweza kuelewa katika Uzazi wa Mpango na pia nimeelewa namna ya upatikanaji wa bima hasa tunapoelekea katika Mapango wa Bima ya Afya kwa Wote na tutakavyonufaika na bima hiyo”amesema kijana Mletwa.

.

 

No comments:

Post a Comment