CORONAVIRUS: TANZANIA YATHIBITISHA KUWA NA KISA CHA KWANZA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 16 March 2020

CORONAVIRUS: TANZANIA YATHIBITISHA KUWA NA KISA CHA KWANZA

Waziri wa Afya Tanzania, Ummy Mwalimu

TANZANIA imethibitisha kisa kimoja cha virusi vya corona.

Mnamo tarehe Machi,15, msafiri huyo aliiingia Tanzania majira ya saa kumi jioni.

Mgonjwa aliyetangazwa ni mwanamke wa miaka 46 raia wa Tanzania, ambaye aliwasili kutoka Ubelgiji kwa ndege ya shirika la Rwanda.

Msafiri huyo aliondoka nchini tarehe 3,Machi 2020 ambapo kati ya tarehe 5-13 Machi alitembelea nchi za Sweden na Denmark na kurudi tena Ubelgiji.

Msafiri huyo alipita uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Waziri Ummy Mwalimu amesema msafiri huyo alipofika KIA alifanyiwa ukaguzi na maafisa wa afya na kuonekana kutokuwa na homa.

Baadae alianza kujisikia vibaya akiwa hotelini na kwenda hospitali ya mkoa ya rufaa ya Mount Meru Arusha ambapo sampuli ilichukuliwa na kupelekwa maabara ya taifa ya afya ya jamii iliyoko Dar es salaam kwa ajili ya uchunguzi.

"Vipimo vya maabara vimethibitisha kuwa mtu huyo ana maambukizi ya ugonjwa wa corona, covid -19, Mgonjwa anaendelea vizuri na matibabu."

Waziri Ummy ameongeza kusema," Serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha kwamba ugonjwa huu unathibitiwa ili usisambae nchini.

Aidha serikali inashirikiana na shirika la afya duniani-WHO na wadau katika kuendelea kutekeleza mikakati ya kukabiliana na ugonjwa huu".

Raia wametakiwa kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huu kadri wanavyopokea taarifa na elimu za mara kwa mara kwa njia mbalimbali.

No comments:

Post a Comment