VIPIMO VYA DNA VILITHIBITISHA UHUSIANO WA HUMPHREY MAKUNDI NA WAZAZI WAKE -SHAHIDI - THE HABARII
  • Home
  • About Us
  • Contact Us

THE HABARII


ASAS GROUP
    • HABARI KITAIFA
    • HABARI KIMATAIFA
    • MICHEZO/BURUDANI
    • HABARI ZA BIASHARA
    • MATUKIO PICHA
    • UCHAMBUZI

    Habari Mpya


    Wednesday, 10 April 2019

    Home Kitaifa VIPIMO VYA DNA VILITHIBITISHA UHUSIANO WA HUMPHREY MAKUNDI NA WAZAZI WAKE -SHAHIDI

    VIPIMO VYA DNA VILITHIBITISHA UHUSIANO WA HUMPHREY MAKUNDI NA WAZAZI WAKE -SHAHIDI

    JOE MUSHI April 10, 2019 Kitaifa,
    Wakili wa kujitegemea David Shiratu wa upande wa utetezi katika shauri la mauaji ya Mwanafunzi, Humphrey Makundi akisalimiana na wateja wake Mahakama kuu, Kanda ya Moshi ambako shauri hilo linaendelea.

    Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande (kushoto) kiteta jambo na baadhi ya watu waliofika mahakamani hapo kwa ajili ya kufuatilia shauri hilo.

    Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande akizungumza jambo na wakili Faygrace Sadallah mara baada ya Mahakama kuahirisha kwa muda usikilizaji wa mashahidi wa upande wa Jamhuri.

    Wakili wa kujitegemea David Shiratu, akifurahia jambo na baadhi ya watu waliofika mahakamani hapo kufuatilia shauri hilo.]


    Na Dixon Busagaga 


    MKEMIA kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Dk. Hadija Mwema ameieleza Mahakama Kuu Kanda ya Moshi  kuwa Vinasaba (DNA) vya sampuli zilizochukuliwa katika mwili wa anayetajwa kama Humphrey Makundi vimeshabihiana na Vinasaba (DNA)  vya Joyce na Jackson Makundi ambao wanatajwa kama wazazi wa marehemu.


    Dk. Mwema ambaye ni shahidi wa 12 katika shauri la mauji ya kukusudia ya Mwanafunzi Humphrey Makundi aliyekuwa akisoma kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Scholastica aliieleza makama kuwa sehemu iliyotoa majibu ya vipimo vya DNA ilikuwa ni Nyama na Nywele katika sehemu ya uume vilivyolinganishwa na Ute wa mate pamoja na Damu vya Joyce na Jackson Makundi.


    Eneo la sehemu ya nyama na Nywele katika eneo la uume ni miongoni mwa sampuli zilizotumika kwa ajili ya vipimo kati ya sampuli 15 ambazo 10 kati ya hizo zilichukuliwa mwilini huku nyingine zikiwa ni viatu na nguo.


    Baadhi ya sampuli nyingine zilizotajwa mahakamani hapo katika ripoti ya vipimo vya DNA ni pamoja na Ngozi ya Kisigino, Mfupa wa Paja, Mfupa wa Kifua, kipande cha nyama ya tako, viatu jozi mbili, maji mazito yanayopatikana katikati ya mfupa vyote hivi vikiwa ni vya marehemu.


    Mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Dar Es Salaam, Firmin Matogoro, shahidi huyo aliiomba Mahakama Kuu Kanda ya Moshi kupokea Ripoti ya Vipimo vya Vinasaba (DNA) iwe sehemu ya kielelezo katika ushahidi wake ambacho kilipokelewa na kupewa namba nne.


    Akiongozwa na Wakili wa serikali Mwandamizi, Abdalah Chavula, Mwema alieza kuwa baada ya kufanya vipimo vya Sampuli mbalimbali matokeo yaliyoonesha zilichukuliwa katika mwili wa Binadamu.


    Mapema Shahidi wa 11 katika shauri hilo linalovuta hisia za watu, Jackson Daudi aliyejitamburisha kama mbebaji wa mizigo katika kiwanda cha kutengeneza Saruji cha Moshi aliwasilisha Panga mahakamani hapo lipokelewe kama kielelezo katika ushahidi wake.


    Akiongozwa na Wakili Mkuu wa Serikali Joseph Pande, Daudi ambaye wakati huo alikuwa akifanya shughuli ya ulinzi katika Shule ya Sekondari ya Scholastica iliyopo Himo katika Wilaya ya Moshi ambako alikuwa akisoma mwanafunzi Humphrey Makundi.


    Alieleza kuwa Novemba 9 mwaka 2017 alifika katika shule hiyo akitokea Kahama, mkoani Shinyanga ambako alifanya kazi ya ulinzi katika kampuni ya Solex Security Ltd kabla ya kukutana na mtu aliyemtaja kama mtoto wa Edward Shayo ambaye alimuunganisha kwenda kufanya kazi katika shule hiyo.


    Daudi aliileza Mahakama sababu za kuacha kazi katika kampuni yake hiyo ya awali ilikuwa ni kutofautiana na muajiri wake baada ya kushindwa kumlipa mshahara wa mwezi mmoja ndipo alipoamua kuchukua vitu katika kampuni yake na kuvipelekea kituo cha Polisi.


    “Baada ya kuelewana na mwajiri wangu na kunipa pesa na kutoka kituoni ,nilikutana na mtoto wa Edward Shayo anaye ishi Wilaya ya Kahama ni Traffic, akaniambia atanipeleka kufanya kazi kwenye shule ya baba yake,” alieleza Daudi.


    Alieleza kuwa Novemba 10, 2017  ikiwa ni siku ya pili tangu kufika shuleni hapo alikutana na  Edward Shayo aliyewauliza kama walielewana bei ya kufanya kazi na majibu yake yalikuwa ni hapana.


    “Alituuliza, mlitaka mlipwe shilingi ngapi? tukamjibu  shilingi laki mbili “alieleza Daudi huku Wakili Pande akitaka kujua walikuwa wangapi ndipo akaeleza kuwa walikuwa wawili yeye na mwenzake aliyemtaja kwa jina moja la Thomas.


    Alieleza kuwa Edward Shayo anayetajwa kama mmiliki wa shule hiyo aliwaambia kuwa atawalipa shilingi laki moja na wao walimueleza kuwa awalipe kiasi cha shs laki moja na ishirini kiwango ambacho alikubaliana nacho na kutoa maelekezo ya kumuona mtu aliyeitwa Chacha.


    “Chacha alikuwa ni mlinzi, baada ya kumuona tukaambiwa nendeni mkapumzike mida ya saa 12 twende tukaonyeshwe eneo la kazi, tulikabidhiwa nguo za kazi," alieleza Daudi.


    Daudi ambye mkewe anafanya kazi ya usafi katika shule ya sekondari ya Scholastica alieleza kuwa utaratibu waliopewa haukuwa wa kulinda wezi na kwamba walilinda wanafunzi wa shule na kwamba hata wangeingia wezi wangepambana nao.


    “Thomas rafiki yangu alibaki pale getini, mimi na Chacha tukaanza kuzunguka maeneo ya shule sikuwa na kitu chochote, Chacha alikuwa akitumia Panga na Rungu," alieleza shahidi huyo.


    Alieleza kuwa Novemba 17, 2017 baada ya kutoka eneo lao la kazi walienda kupumzika na Chacha  na baadae mtu aliyemtaja kwa jina la Mcha Mungu liyekuwa mlinzi wa getini  alifika na kuwaita bila ya kuwaeleza kuwa wanaitwa na nani.


    “Tuliendelea kulala, Mchamungu akatuita mara ya pili ,akaita tena Chacha Chacha mnaitwa ,tukaulizwa tunaitwa na nani? Akatuanmbia mnaitwa na maaskari ,tukaenda getini tukakuta askari wa kike “trafiki “ “alieleza Daudi.


    Shahidi huyo alieleza kuwa baada ya kufika yule Askari aliuliza anaitwa nani ndipo alipomtajia majina yake ya Jackson Evarlist Daudi na kueleza kuwa sio yeye huku akiuliza Chacha ni nani.


    “Alipouliza Chacha nikamnyooshea kidole huyo hapo, akauliza na Mchamungu? Nikamnyooshea kidole huyo hapo na siku hiyo ilikuwa ni zamu ya Mchamungu kukaa getini” alieleza Daudi.


    Mnamo Novemba 18 ,2017 majira ya saa mbili za usiku ,Daudi alieleza kuwa ilifika gari aina ya Landcruser ikiwa na vioo vyeusi ndipo alipofungua mlango mdogo katika geti la kuingia shuleni hapo ndipo aliposikia sauti ikimueleza kuwa hawaingii ndani.


    “Walikuwa ni maaskari wakafungua mlango wa gari, wakamtoa Chacha, Chacha akwaongoza maaskari paka pale Panga lilipokuwa ,Panga lilikuwa kwenye kabati ndani ya Chumba cha Mlinzi, kilichopo geti kuu la kuingia shuleni”alieleza Daudi.


    “Walivyokuta Panga askari wakaniuliza tangu nifike hapo sijawahi kulishika hilo Panga au kulikamata nikasema hapana, nikaulizwa Panga la nani? Chacha mwenyewe kwa kinywa chake akakili Panga la kwangu,” aliongeza Daudi.


    Alieleza kuwa kuna Rungu lilikuwa juu ya meza ambapo pia askari walitaka kujua endapo nimewahi kulishika na majibu yalikuwa ni hapana na kwamba baada ya hapo walipiga picha Panga na Rungu kisha wakaongozana na Chacha wakiwa na vitu hivyo.


    Daudi alieleza muonekano wa Panga ulikuwa wa rangi nyeusi huku likiwa imemeguka kidogo huku akiionesha mahakama Panga hilo na baadae kuiomba mahakama itoe adhabu kutokana na Panga hilo.


    Baada ya kutoa maelezo hayo Wakili Mkuu wa Serikali ,Pande aliwasilisha ombi mbele ya mahakama kupokea Panga hilo liwe sehemu ya kielelezo katika ushaidi wa Daudi jambo ambalo lilizua mabishano ya kisheria kwa pande zote mbili.


    Wakili wa kujitegemea, Gwakisa Sambo akiwasilisha ombi kwa Jaji, Mfawidhi, Matogoro alieleza kupinga ombi hilo akieleza sababu ya kuwa Wakili Pande si shahidi wa kutoa kielelezo hicho.


    “Maombi yetu kwa upande wa prosecutor, ni mahakama hii na mahakama zetu nchini ni shahidi pekee yake ambaye anaweza kuleta ombi hilo, hivyo basi tunaomba ombi lake likataliwe.


    Baadae alisimama wakili Pande na kuunga mkono hoja ya Wakili Sambo huku akileza kuwa ni kweli anayetoa kielelezo ni shahidi lakini anayeomba kielelezo kipokelewe ni upande wa Jamhuri na kwamba hivyo ni vitu viwili tofauti.


    Shauri hilo linaendelea katika Mahakama Kuu Kanda ya Moshi,ambapo mashahidi wa upande wa jamhuri wameendelea kuwasilisha ushahidi wao.


    Shauri la mauaji  ya mwanafunzi  Humphrey Makundi aliyekuwa akisoma kidato cha pili katika  sekondari ya Scolastika imeanza kusikilizwa mfululuzo  likimkabili mmiliki wa shule hiyo ,Edward Shayo,Mwalimu wa nidhamu Labani  Nabiswa  na mlinzi wa shule ,Hamis Chacha.


     Upande wa Jamhuri katika Shauri hilo unawakilishwa na Wakili wa serikali Mkuu ,Joseph Pande,Wakili wa serikali Mwandamizi ,Abdala Chavula,Wakili wa serikali Mwandamizi ,Omary Kibwana  na Wakili wa serikali Lucy Kiusa.


    Upande wa utetezi unawakilishwa na Wakili wa kujitegemea Elikunda Kipoko na Gwakisa Sambo wanaomtetea  mshtakiwa wa pili ,Wakili wa kijitegemea David Shilatu anayemtetea mshitakiwa wa kwanza na Patrick Paul anaye mtetea mshtakiwa wa tatu.






    Tags # Kitaifa
    Share This
    Author Image

    About JOE MUSHI

    Kitaifa
    By JOE MUSHI at April 10, 2019
    Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
    Labels: Kitaifa

    No comments:

    Post a Comment

    Newer Post Older Post Home
    Subscribe to: Post Comments (Atom)

    Author Details

    Joachim Mushi| Mwenyekiti Tanzania Bloggers Network (TBN) | Mhariri Mkuu wa TheHabarii. | Mail:mushijoa@gmail.com | +255 717 030 060 / +255 756 469 470.

    Socialize

    • facebook count=3.5k;
      Followers
    • twitter count=1.7k;
      Followers
    • youtube count=2.8k;
      Followers
    • instagram count=849;
      Followers

    Blogu Marafiki

    • JIACHIE
      WIZARA YA AFYA YASIKITISHWA NA WANAOTAPELI KWA JINA LA MCHENGERWA - WIZARA ya Afya imesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu wenye nia ovu ambao wamekuwa wakitumia jina la Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa k...
      7 hours ago
    • MTAA KWA MTAA BLOG
      WIZARA YA AFYA YASIKITISHWA NA WANAOTAPELI KWA JINA LA MCHENGERWA - WIZARA ya Afya imesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu wenye nia ovu ambao wamekuwa wakitumia jina la Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa k...
      7 hours ago
    • MICHUZI BLOG
      WIZARA YA AFYA YASIKITISHWA NA WANAOTAPELI KWA JINA LA MCHENGERWA - WIZARA ya Afya imesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu wenye nia ovu ambao wamekuwa wakitumia jina la Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa ku...
      7 hours ago
    • Father Kidevu
      AFRICACUP SPINNERS ZAZINDULIWA MUBASHARA betPawa WAKATI AFCON INAPAMBA MOTO - *Dar es Salaam. Kadri mashindano makubwa ya soka barani Afrika yanavyoendelea kupamba moto mwezi huu, mashabiki kote barani wanaingia kwenye msisimko wa ...
      3 days ago
    • Wazalendo 25 Blog
      Habari : Serikali yasisitiza Usalama ,Mapato Mpakani Mutukula - Na Mwandishi Wetu,KAGERA Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amehimiza ushirikiano kati ya watumishi wa serikali waliopo katika Kituo ch...
      4 days ago
    • THE HABARII
      NAIBU WAZIRI WA ELIMU ATEMBELEA NIT.MSAADA MKUU - *NA DUNSTAN MHILU* *NAIBU* Waziri wizara ya Elimu ya Juu Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidhi Ameir amesema amelidhishwa na utekelezaji wa miradi ya miund...
      1 week ago
    • Millardayo.com
      Habari kubwa Magazetini Kenya leo March 3, 2025 - Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania March 3, 2025,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma Magazetini ke...
      9 months ago

    Zinazotembelewa Zaidi

    • SERIKALI KUZIFANYIA KAZI CHANGAMOTO ZA WAANDISHI WA HABARI ZA MITANDAO
      SERIKALI KUZIFANYIA KAZI CHANGAMOTO ZA WAANDISHI WA HABARI ZA MITANDAO
      Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa akizungumza na waandishi wa haba...
    • NAIBU WAZIRI WA ELIMU ATEMBELEA NIT.MSAADA MKUU
      NAIBU WAZIRI WA ELIMU ATEMBELEA NIT.MSAADA MKUU
      NA DUNSTAN MHILU NAIBU  Waziri wizara ya Elimu ya Juu Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidhi Ameir amesema amelidhishwa na utekelezaji wa mirad...
    • MAJIKO BANIFU YA RUZUKU YAPIGA HODI KATAVI
      MAJIKO BANIFU YA RUZUKU YAPIGA HODI KATAVI
        MKUU wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wa Katavi kuchangamkia fursa ya kununua majiko banifu kwa bei ruz...
    •  NMB YAJA NA MABORESHO YA HUDUMA KWA MAKANDARASI WA ZANZIBAR
      NMB YAJA NA MABORESHO YA HUDUMA KWA MAKANDARASI WA ZANZIBAR
      Na Mwandishi Wetu, Zanzibar  KATIKA kuendelea kuimarisha sekta ya ujenzi visiwani Zanzibar, Benki ya NMB imezindua maboresho ya masuluhisho...
    • RAIS MHE. DKT. SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA, DAR
      RAIS MHE. DKT. SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA, DAR
      Mbunge wa Jimbo la Nachingwea Fadhili Liwaka akitoa ahadi ya kuwalipia bodaboda zaidi 300 shilingi Elfu tano (5000) kwa Kila bodaboda atakay...
    •  WADAU SEKTA YA USAFIRISHAJI WAKIHAKIKISHIA USHIRIKIANO CHUO CHA NIT
      WADAU SEKTA YA USAFIRISHAJI WAKIHAKIKISHIA USHIRIKIANO CHUO CHA NIT
      Mgeni Rasmi katika kongamano la 12 la kitaaluma la NIT, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Superdol , Jamal Bayser akimkabidhi mmoja wa wanafunzi ...
    • RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA, IKULU DAR
      RAIS DKT. SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. JAJI JOSEPH SINDE WARIOBA, IKULU DAR
        Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Jaji Joseph...
    • KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI, AFUNGA KIKAO KAZI CHA KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS NA MAAFISA HABARI WA SERIKALI
      KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI, AFUNGA KIKAO KAZI CHA KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS NA MAAFISA HABARI WA SERIKALI
        Mkurugenzi wa Pioneer Communications Salva Rweyemamu akizungumzia mada yake ya Utayari wa Mawasiliano wakati wa migogoro na majanga katika...
    • KM SANGA AIPONGEZA TUME YA TAIFA YA MATUMIZI YA ARDHI KWA UPANGAJI NA USIMAMIZI WA ARDHI NCHINI
      KM SANGA AIPONGEZA TUME YA TAIFA YA MATUMIZI YA ARDHI KWA UPANGAJI NA USIMAMIZI WA ARDHI NCHINI
      Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo akimkabidhi vitendea kazi mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Mi...
    • RAIS DKT. SAMIA AZUNGUMZA NA BALOZI WA KENYA TANZANIA ANAYEMALIZA MUDA WAKE MHE. NJENGA IKULU DAR
      RAIS DKT. SAMIA AZUNGUMZA NA BALOZI WA KENYA TANZANIA ANAYEMALIZA MUDA WAKE MHE. NJENGA IKULU DAR
        Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Kenya nchini Tanzania anayemaliza muda wak...

    Facebook

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Recent

    Comments

    Kumbu Kumbu

    Maktaba

    Kitaifa MATUKIO PICHA Biashara KIMATAIFA UCHAMBUZI Burudani MATUKIO PICH EVENTS PHOTO NATIONAL PHOTO MATUKIO MAKALA PICH
    • Home
    • About Us
    • Contact Us

    Zinazotembelewa Zaidi

    • MATOKEO YA KURA ZA MAONI ZA CCM MAJIMBO MBALIMBALI
      Bw. Anthony Mavunde ashinda Jimbo la  Dodoma Mjini   kwa kupata kura 904. Mtoto wa Stiven Wasira akisaini fomu ya matokeo baada ya b...
    • SERIKALI YARUDISHA HAZINA BILIONI TATU ZA MRADI WA KIMKAKATI WA MACHINJIO YA VINGUNGUTI
      Afisa Mipango wa Manispaa ya Ilala Bw. Ando Mwankuga, akitoa maelezo ya ujenzi wa Soko la Kisutu Jijini Dar es Salaam, mradi ambao ni wa k...
    • KATIBU MKUU TAMISEMI, ENG NYAMHANGA AKABIDHI OFISI
      Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Eng. Joseph Nyamhanga akimpongeza Katibu Mkuu mpya wa Wizara ya U...

    Zinazobamba Zaidi

    • SERIKALI KUZIFANYIA KAZI CHANGAMOTO ZA WAANDISHI WA HABARI ZA MITANDAO
      Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa akizungumza na waandishi wa haba...
    • NAIBU WAZIRI WA ELIMU ATEMBELEA NIT.MSAADA MKUU
      NA DUNSTAN MHILU NAIBU  Waziri wizara ya Elimu ya Juu Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidhi Ameir amesema amelidhishwa na utekelezaji wa mirad...
    • MAJIKO BANIFU YA RUZUKU YAPIGA HODI KATAVI
        MKUU wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wa Katavi kuchangamkia fursa ya kununua majiko banifu kwa bei ruz...

    Zilizoshika Sana

    • DKT. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAZI CHA WAKUU WA MIKOA
      WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 27, 2025 ameongoza kikao cha kazi cha Wakuu wa Mikoa Tanzania bara, kikao hicho kimefanyika Of...
    • TBN YATOA UFAFANUZI KUHUSU MKUTANO WA IKULU NA KURUGENZI YA MAWASILIANO
      Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bw. Bakari Machumu akizungumza na Waandishi wa Habari wa Mtandaoni pamoja na Wanablogu mbalimbali,...
    • VERONICA MREMA WA TBN AINGIA JOPO LA MDAHALO MKUTANO MKUU WA DUNIA WA WAANDISHI WA SAYANSI
      PRETORIA, AFRIKA KUSINI KILELE cha utambuzi wa uandishi wa habari za kidijitali nchini Tanzania kimethibitishwa baada ya Bi. Veronica Mrema...

    Contact Form

    Name

    Email *

    Message *

    Designed By By The Habari | Developed by Gadiola Emanuel