MAHAFALI YA MWAKA 2019 SUZA YAMEANDIKA HISTORIA-PROF. RAI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 24 April 2019

MAHAFALI YA MWAKA 2019 SUZA YAMEANDIKA HISTORIA-PROF. RAI

Prof Idissa Rai 


Na Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar

MAKAMU  Mkuu wa Chuo cha Taifa Zanzibar (SUZA) Prof Idissa Rai amesema mahafali ya mwaka huu yameandika historia mpya kwa Chuo hicho kutowa wahitimu wa fani ya Udaktari hapa nchini. Prof. Rai amesema hayo katika hafla ya Mahafali ya 14 ya SUZA yaliofanyika katika viunga vya Chuo hicho Tunguu, Mkoa wa Kusini Unguja.

Alisema uanzishaji wa masomo hayo  ni utekelezaji wa agizo la Rais alilolitowa katika mahafali ya mwaka 2011, kwa lengo la kuhakikisha Zanzibar inajitegeme kwa wataalamu wa  fani nhiyo. Alisema hatua ya Chuo hicho kutowa wahitimu 25 wa fani hiyo inatowa muelekeo mzuri wa kufikia malengo hayo.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwapongeza Dk. Mohamed Jidawi na Dk. Jamala kwa mchango mkubwa iliofanikisha kuanzishwa kwa fani hiyo chuoni nhapo. Pro. Rai, aliipongeza Serikali ya watu wa Cuba kwa mashirkiano na mchango mkubwa uliowezesha kufanyika kwa mafunzo hayo.

Alisema baada ya Serikali kufikia uamuzi wa kukiimarisha chuo hicho na kukiunganisha na taasisi mbali mbali, chuo kilichukuwa hatua za kuanzisha masomo katika fani mpya pamoja na kuweka vipaumbele na mikakati madhubuti.

Alisema mambo muhimu yaliozingatiwa kufanikisha malengo hayo ni pamoja na kujenga uwezo kwa wanataaluma , kujenga miundombinu mipya na kukarabati ile iliopo ili iendane na fani husika. Alisema hivi sasa chuo kimo katika maandalizi ya kuanzisha fani ya Udaktari wa meno, sambamba na malengo ya baadae ya kuanzisha masomo ya Ubaharia.

Aidha, alisema Progaramu ay kazi ya mafunzo ya Utalii, ina lengo la kutoa taswira nzuri ya shughuli  za utalii ili kupanuwa wigo wa ajira kwa vijana wa Kizanzibari kupitia sekta hiyo. Aliupongeza uongozi na wahadhiri wa chuo hicho kwa kazi kubwa wanayofanya kwa maendeleo ya chuo hicho.

“Uongozi wa Chuo unathamini sana juhudi zenu,tuongeze bidii katika kazi zetu na kuzidisha uzalendo kwa nchi yetu, ili changamooto mbali mbali zinazotukabili zisiwe kikwazo katika kufikia Dira na dhamira za chuo”, alisema Pro. Rai.

Nae, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu an Mafunzo ya Amali Dk. Idrissa Muslih Hija, kwa niaba ya Mwenyekiti wa Baraza hilo,  alisema mahafali ya mwaka huu imepanua wigo kwa kuongezeka fani mbili zaidi, tofauti na mwaka uliopita.

Alizitaja fani zilizoongezeka ni  pamoja na Shahada ya Udaktari (doctor of Medicine) pamoja na Cheti cha uanagenzi (certificate of Apprentenship  katika masuala ya Utalii.
Alisema hatua hiyo imetowa matumaini ya kuongezeka kwa idadi ya madaktari katika Hospitali hapa nchini, na kuondokana an tatizo la uhaba wa madaktari uliopo.
Alisema fani hizo ni muhimu katika kuimarisha maendeleo ya nchi na ustawi wa watu wake, kwani mafunzo waliyoyapata yalizingatia mahitaji ya jamii.
Dk. Idrisa alitumia fursa hiyo kuwapongeza washirika wa maendeleo kwa juhudi na mchango wao mkubwa katika kukiendeleza Chuo hicho kupitia nyanja tofauti.
Alizitaja taasisi na mashirika hayo kuwa ni pamoja na Milele Foundation. UNICEF,World Bank, NORAD, DANIDA, HUAWEI, Ubalozi wa Uturuki, Serika ya Watu wa China  pamoja na Falme za Kiarabu.

Nae, Waziri wa Elimu na Mafgunzo ya Amali, Riziki Pembe Juma aliipongeza serikali kw ajuhudi kubwa inazoendelea kuchukuwa kuiendeleza sekta ya elimu nchini, ikiwemo ya elimu ya juu.

Alisema hatua ya Serikali kuongeza bajeti ya upatikanaji wa mikopo ya elimu ya juu kutoka shilingi Bilioni 6.8 hadi Bilioni 11 imetowa fursa ya kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kupata mikopo hiyo


No comments:

Post a Comment