NCHI 23 ZA BARA LA AFRIKA WASHIRIKI MAFUNZO YA HALI YA HEWA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 15 August 2018

NCHI 23 ZA BARA LA AFRIKA WASHIRIKI MAFUNZO YA HALI YA HEWA

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dk. Agnes Kijazi.


Na Ahmed Mahmoud, Arusha

SHIRIKA la Hali ya Hewa Duniani (WMO) kwa kishirikiana na Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA) wameandaa mafunzo kwa nchi 23 za Afrika ya utumiaji wa mfumo wa Teknolojia ya kuboresha huduma za utabiri wa hali ya hewa ambao utasaidia kujua maeneo yasiona vituo.

Akizungumza jana Jijini hapa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dk. Agnes Kijazi wakati wa ufunguzi wa warsha ya mafunzo hayo, alisema mfumo huo utawezesha utoaji wa taarifa sahihi zahali ya hewa .

Alisema kuwa mbali na kuboresha utoaji wataarifa pia wataweza kubaini maeneo ambayo hayana vituo na kuweza kuongeza kwa ajili ya kutoa taarifa zenye uhalisia.

Dk. Kijazi alisema mafunzo hayo yamekuja mahususi nchini kwa ajili ya kuwanoa wataalamu wa nchi za Afrika ili waweze kutumia mfumo huo vema.

"Kwa mfano hapa Tanzania tuna vituo vya aina nyingi kama vya rada tunavyo viwili tunahitaji saba na Vituo vinavyojiendesha vyenyewe  36 katika mikoa mbalimbali ikiwemo Arusha, lakini kama nchi tunahitaji kama 100,"alisema

Alisema pia kwa upande wa vituo vya upimaji wa mvua tunavyo 300 lakini mahitaji ni 2500,hivyo uhitaji mkubwa na kwa kutumia mfumo huo mpya wataweza kuongeza vingine zaidi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo alisema mafunzo hayo ni muhimu,kwani yanawezesha wataalamu kubaini hali halisi ya mabadiliko ya tabia ya nchi na jinsi ya kukabiliana nayo na hivyo kuongeza tija na katika utendaji wataasisi hiyo.

Amesema kuwa hapa nchini na mkoa wa Arusha kumekuwa na mabadiliko ya Tabianchi hususani maeneo ya longido ambapo serikali imekuwa ikisaidia kwa karibu katika kuhakikisha masuala yote yanaenda sawa katika suala zima la kupambana na mabadiliko hayo.

"Taarifa za hali ya hewa ni muhimu kwa wananchi ili waweze kufanya  uamuzi sahihi kwa shughuli zao mbalimbali," alisema.

No comments:

Post a Comment