LEO Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefungua Skuli ya Maandalizi ya Tasani ikiwa ni muendelezo wa mchango wa Benki ya NMB katika kuchangia ukuaji wa elimu nchini.
Kwa kutambua mchango wa Serikali ya
Awamu ya Sita katika kuinua sekta ya elimu nchini, shule hiyo imepewa jina la Dkt.
Samia Suluhu Hassan.
Katika ufunguzi wa shule hii, Afisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna alimueleza Mheshimiwa Rais
kuwa:
✅ Benki ya NMB
imegharamia ujenzi wa skuli hii na uwekaji wa samani (ikiwemo viti, meza na
madawati) kwa asilimia 💯 kwa gharama ya Shilingi Milioni 800.
✅ Skuli ina madarasa
matano na itaweza kupokea wanafunzi 200 kwa wakati mmoja. Pia imejumuisha ofisi
za waalimu, sehemu ya michezo ya watoto na miundombinu mingine.
Tukiwa wadau wa karibu wa maendeleo
nchini, tunaamini skuli hii itahudumia vizazi ambavyo kwa baadae vitakuja
kuleta mchango mkubwa katika maendeleo ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
No comments:
Post a Comment