KATIBU MKUU MHE. ABDULLA, AKAGUA VIFAA VYA UPANUZI MKONGO WA TAIFA WA MAWASILIANO AWAMU YA III - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Thursday 21 September 2023

KATIBU MKUU MHE. ABDULLA, AKAGUA VIFAA VYA UPANUZI MKONGO WA TAIFA WA MAWASILIANO AWAMU YA III

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mohamed Khamis Abdulla akitoa maelekezo mara baada ya kukagua vifaa vya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano, awamu ya III sehemu ya ii, vilivyowasili tayari kwa utekelezaji wa zoezi hilo.


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mhandisi Peter R. Ulanga (kulia) akioa maelezo ya vifaa vilivyowasili kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano, awamu ya III sehemu ya ii, vilivyowasili tayari kwa utekelezaji wa zoezi hilo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mhandisi Peter R. Ulanga (kulia) akifafanua jambo mara baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mohamed Khamis Abdulla kukagua vifaa vya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano, awamu ya III sehemu ya ii, vilivyowasili tayari kwa utekelezaji wa zoezi hilo.

Sehemu ya vifaa vya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano, awamu ya III sehemu ya ii, vilivyowasili tayari kwa utekelezaji wa zoezi hilo vikiwa eneo la Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya vifaa vya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano, awamu ya III sehemu ya ii, vilivyowasili tayari kwa utekelezaji wa zoezi hilo vikiwa eneo la Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Timu ya wakandarasi wa HUAWEI anaotarajiwa kutekeleza mradi huo akiwa tayari kwa kazi hiyo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mhandisi Peter R. Ulanga akioa maelezo ya mradi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mohamed Khamis Abdulla (hayupo pichani) mara baada ya kukagua vifaa vya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano, awamu ya III sehemu ya ii, vilivyowasili tayari kwa utekelezaji wa zoezi hilo.

Timu ya Wasimamizi wa Miradi (Project Manager) ambao watakuwa na jukumu la kuhakikisha wanasimamia mradi huo kikamilifu na kwa kuzingatia weledi ikifuatilia hotuba ya Katibu Mkuu mara baada ya ziara yake.

Na Joachim Mushi, Dar  

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mohamed Khamis Abdulla leo amekagua vifaa vya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa mkongo wa taifa wa mawasiliano, awamu ya III sehemu ya ii, vilivyowasili tayari kwa utekelezaji wa zoezi hilo.

Akizungumza katika tukio hilo, Bw. Khamis Abdulla amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mhandisi Peter R. Ulanga kuhakikisha mradi huo unatekelezwa kwa wakati na katika thamani halisi kwa mujibu wa makubaliano.

Alisema Serikali imeliamini Shirika la TTCL na kuliwezesha ili kuhakikisha linatekeleza kikamilifu mradio huo, unaokwenda kuchochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini Tanzania.

Kwa upande wake, Mhandisi Ulanga alisema kwa kuweka umuhimu mradi huo, umeandaa Timu ya Wasimamizi wa Miradi (Project Manager) ambao watakuwa na jukumu la kuhakikisha wanasimamia miradi kikamilifu na kwa kuzingatia weledi.

“Tumewapatia vitendea kazi ikiwemo magari kwa kila Msimamizi wa Mradi ili kurahisisha shughuli katika kutekeleza miradi hiyo. Na bahati nzuri katika tukio hili leo timu ya  Wasimamizi wa Miradi wako hapa.

“Shirika la Mawasiliano Tanzania tuko tayari kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita, ikiongonzwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha miradi wa kuunganisha Wilaya zote nchi nzima  katika Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano inatekelezwa kikamilifu.

Akifafanua zaidi alisema TTCL iko tayari kushirikiana na Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imefanikisha katika kukamilisha miradi yote ya mawasiliano. Tunatambua dhamira ya Serikali katika kuwafikisha mawasiliano Watanzania yenye ubora na yenye Uhakika,” alisema Mkurugenzi huyo.

Akitoa ufafanuzi wa taarifa ya utekelezaji wa Upanuzi wa mradi huo wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano Awamu ya Tatu, Sehemu ya Pili alibainisha kuwa Upanuzi utafanyika katika Wilaya 32.

“Upanuzi huu unahusisha kufikisha Mkongo wa Taifa kwenye Wilaya 32, huku Wilaya 23 za mradi huu ziko chini ya Mkandarasi wakati upanuzi kwenda Wilaya 9 unafanywa na wataalamu wa ndani wa TTCL pamoja na upanuzi wa mzunguko wa Kaskazini na Magharibi kutoka 800Gbps hadi 2 Tbps.

No comments:

Post a Comment