RAIS DK.SAMIA SULUHU HASSAN AIPA TANO MSD KWA UFANISI WA KAZI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday 19 August 2023

RAIS DK.SAMIA SULUHU HASSAN AIPA TANO MSD KWA UFANISI WA KAZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Dk.Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye ufunguzi wa Kikao Kazi kwa Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma kilichoandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Jukwaa la Wakuu wa Taasisi za Umma, kilichofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa AICC Jijini Arusha tarehe 19 Agosti, 2023.

 Na Mwandishi Wetu, Arusha

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan ameridhishwa na mabadiliko yanayoendelea Bohari ya Dawa ( MSD) na kuwataka waendeleee kuchapa kazi.

Rais Samia amesema hayo  Jumamosi Agosti 19, 2023 jijini Arusha wakati akifungua kikao kazi cha wenyeviti wa bodi na taasisi za umma.

Rais Dk.Samia akiwa amemsimamisha Mkurugenzi wa MSD, Mavere Tukai alisema taasisi hiyo ni kati ya mashirika yaliyo badilika na matumaini yake itakwenda kufanya vizuri hasa katika mfumo wa  uuzaji wa Dawa Afrika kwa kuwa na soko kubwa hususani kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC).


No comments:

Post a Comment