ROYAL TOUR' YA RAIS SAMIA SULUHU YAANZA KUZAA MATAUNDA NCHINI, WAWEKEZAJI WAANZA KUMIMINIKA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Thursday 23 September 2021

ROYAL TOUR' YA RAIS SAMIA SULUHU YAANZA KUZAA MATAUNDA NCHINI, WAWEKEZAJI WAANZA KUMIMINIKA

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waongoza Watalii nchini Bulgaria ambaye pia ni Mkuu wa Msafara wa Wawekezaji,   Lachezar Todorov akimkabidhi Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro moja ya zawadi mara baada yq kufanya mazungumzo na Wawekezaji  mahiri kutoka Taifa la Bugaria ambao wanakusudia kujenga hoteli nne zenye hadhi ya nyota Tano katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Manyara , Tarangire na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro katika mkutano  wake maalum na  Wawekezaji hao uliofanyika Jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro (wa nne kulia)  akiwa kwenye picha ya pamoja na Wawekezaji  mahiri kutoka Taifa la Bulgaria ambao wanakusudia kujenga hoteli nne zenye hadhi ya nyota Tano katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Manyara Tarangire na Malmlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro mara baada ya   mkutano  wake maalum na  Wawekezaji hao uliofanyika Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waongoza Watalii nchini Bulgaria,   Lachezar Todorov na kulia wa nne ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo , Dkt.Allan Kijazi.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt.Allan Kijazi (kulia) wakizungumza na  Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waongoza Watalii nchini Bulgaria Lachezar Todorov ambaye pia ni Mkuu wa Msafara wa Wawekezaji  kutoka Taifa la Bugaria,  ambao wanakusudia kujenga hoteli nne zenye hadhi ya nyota Tano katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Manyara Tarangire na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro katika mkutano  wake maalum na  Wawekezaji hao uliofanyika  leo Jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Maalum

SHUGHULI za Royal Tour zilizokuwa zikifanywa kwa mara ya kwanza nchini na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan za kutangaza vivutio vya Utalii, Biashara na Uwekezaji nchini zimeanza kuzaa matunda kwa wawekezaji kuanza kujitokeza kwa uwekezaji wa hoteli za kisasa ndani ya hifadhi za Taifa.

Hayo yamebainishwa na Serikali kupitia kwa Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro mara baada ya mkutano  wake maalum na  Wawekezaji uliofanyika Dar es Salaam mapema leo. Ambapo amekutana na wawekezaji hao kutoka Bara la Ulaya katika nchi ya Bulgaria watakaojenga hotel za Nyota tano 'brand'  za Kempinski kwenye hifadhi Nne za Taifa nchini.

Waziri Dk. Damas Ndumbaro amesema mpango mkakati wa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kupitia kuandaa kipindi cha Royal Tour umeweza kuzaa matunda hayo na wao kwa Wizara wameupokea kwa kwa sasa ni utekelezaji.

''Juhudi kubwa za kimkakati za Royal Tour zilizoendeshwa na Rais wetu zimeweza kuzaa matunda ambapo leo tumepokea wawekezaji mahiri kutoka Bara la Ulaya ambao watawekeza kwenye hoteli kwa kujenga hoteli tatu za nyota tano za 'brand'  ya  Kempinski  kwa uwekezaji wa Dola za Kimarekani Milioni 72. [USD 72 Milioni].

''Mkutano wetu huu hii leo umekwenda vizuri sana na Wawekezaji hawa  kwa hiyo unaweza kuipata hoteli ya Kempinski baada ya ujenzi huo kukamilika. .. Kempinski Serengeti,  Kempinski Manyara, Kempinski Tarangile na Kempinski Ngorongoro." Alisem Dk. Ndumbaro.

Waziri Dkt. Ndumbaro ameongeza kuwa,  ujenzi huo ni mkubwa sana  na unakadiriwa kuanza rasmi mwezi Januari 2022 ambapo amemshukuru  kwa mara nyingine Mhe Rais kwa kuwezesha kuwapigia 'pass' na wao kupitia wizara ya Maliasili ni utekelezaji ikiwemo kupokea Wawekezaji katika sekta hiyo ya Utalii.

''Tunaenda kasi tayari hii Royal tour  kwangu mimi kama Waziri  na Wizara ya Utalii na Maliasili kwa ujumla wake tunaichukulia kama 'pass' ya mwisho katika mpira, unapopewa pasi ya mwisho kazi yako wewe ni kufunga tu. Kwa hiyo sisi tumeshafunga 'Goal' lingine hilo kuhakikisha kwamba Royal Tour inakuwa na mafanikio zaidi'' alimalizia Waziri Dkt. Damas Ndumbaro.

Agosti 28,  mwaka huu Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan  alianza rasmi kurekodi vipindi vya Royal Tour maeneo mbalimbali ya vuvutio vya utalii na uwekezaji ikiwemo Tanzania Bara na visiwa vya Zanzibar. Ambapo katika ziara hiyo ya kuandaa vipindi hivyo kutembelea na kuonesha kwa wageni vivutio mbalimbali vya Utalii, Uwekezaji, Sanaa na Utamaduni vilivyopo nchini na kwa sasa matunda yake yameanza kuonekana.


Baadhi ya Wawekezaji  mahiri kutoka Taifa la Bulgaria ambao wanakusudia kujenga hoteli tatu zenye hadhi ya nyota Tano katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Manyara na Tarangire na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongror wakimsikiliza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro katika mkutano  wake maalum na  Wawekezaji hao uliofanyika Jijini Dar es Salaam. Uwekezaji huo ni matokeo ya kampeni ya kutangaza vivutio vya utalii nchini kupitia kipindi cha Royal Tour alichokiasisi Rais Mhe.Samia Suluhu Hassam.

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro akizungumza na  Wawekezaji  mahiri kutoka Taifa la Bulgaria ambao wanakusudia kujenga hoteli tatu zenye hadhi ya nyota Tano za 'brand' ya Kempinski katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Manyara Tarangire na Mamlaka ya Eneo la  Hifadhi ya Ngorongoro,  ikiwa ni matokeo ya Kampeni ya Royal Tour iliyoasisiwa na Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan,  katika mkutano  wake maalum na  Wawekezaji hao uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment