MAJALIWA ASHUHUDIA UTIAJI SAIN WA UJENZI WA BARBARA YA NANGANGA- RUANGWA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday 28 June 2020

MAJALIWA ASHUHUDIA UTIAJI SAIN WA UJENZI WA BARBARA YA NANGANGA- RUANGWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Elias Kuandikwa wakishuhudia wakati Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania(TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale na Mwakilishi wa Kampuni ya China  Railway 15 Bureau Group Corporation, Su Jinlan  wakitia saini mkataba wa makubaliano kati ya serikali na Kampuni hiyo ya ujenzi wa barabara ya Nanganga -Ruangwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Kilomita 53.2 kwa gaharama ya Sh. Bilioni 59.28. Utiaji saini wa Mkataba huo ulifanyika kwenye uwanja wa Likangala , Ruangwa, Juni 27, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TAROADS), Mhandisi Patrick Mfugale na Mwakilishi wa Kampuni ya China  Railway 15 Bureau Group Corporation, Su Jinlan  wakibadilishana  nakala za mkataba wa makubaliano kati ya serikali na Kampuni hiyo wa ujenzi wa barabara ya Nanganga -Ruangwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Kilomita 53.2 kwa gaharama ya Sh. Bilioni 59.28. Mkataba huo ulitiwa saini  na kushuhudiwa na Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa kwenye uwanja wa Likangala, Ruangwa Juni 27, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale (kulia) na Mwakilishi wa Kampuni ya China  Railway 15 Bureau Group Corporation, Su Jinlan  wakionyesha nakala za mkataba wa makubaliano kati ya serikali na Kampuni hiyo ya ujenzi wa barabara ya Nanganga -Ruangwa yenye urefu wa Kilomita 53.2 kwa  gaharama ya Sh. Bilioni 59.28. Mkataba huo ulitiwa saini  huku ukishuhudiwa na Waziri Mkuu ambaye pia ni Mbunge wa Ruangwa kwenye uwanja wa Likangala, Ruangwa Juni 27, 2020. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

No comments:

Post a Comment