WATUHUMIWA UJAMBAZI WAKAMATWA KABLA KUFANYA UHALIFU ARUSHA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Friday 8 May 2020

WATUHUMIWA UJAMBAZI WAKAMATWA KABLA KUFANYA UHALIFU ARUSHA

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Jonathan Shana akiongozana na Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo mwenye Suti ya blue wakitoka kukagua gari Lilikuwa likitumiwa na majambazi hao aina ya Toyota Crown lenye namba za usajili T777DSJ wakati akitoa taarifa ya kukamatwa kwa majambazi wanne jijini Arusha picha zote na Ahmed Mahmoud Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akilipongeza Jeshi la Polisi kwa kutumia sheria ya tii bila shuruti na kufanikiwa kukamata majambazi wanne bila kuwapiga risasi baada ya kutii bila shuruti usiku wa kuamkia jijini Arusha.
M
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akionyeshwa gari aina ya Toyoto Crown lililokuwa na majambazi waliokuwa njiani kuja kufanya matukio ya kiuhalifu mkoani Arusha.

Sehemu ya mbele ya Gari hilo kama lilivyokutwa na kamera ya matukio jijini Arusha picha zote na Ahmed Mahmoud Arusha.

JESHI la Polisi Mkoa wa Arusha baada ya upata taarifa fiche limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne wa ujambazi akiwemo Mganga wa Kienyeji wakiwa na silaha mbili za Moto kwa ajili ya kuja kufanya matukio ya kiuhalifu mkoani hapa.

Akizungumza na vyombo vya habari mkoani hapa Kamanda wa Polisi, Jonathan Shana amesema jeshi limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa; Steven Godfrey (32) mkazi wa Tabata, Yunusi Hamed (37) mkazi wa Tanga, Said Hamisi (38) mkazi wa Dar es salaam pamoja na Msafiri Yohana (22) mkazi wa Mwanza.

Mnamo tarehe 6 mwezi wa tano mwaka huu majira ya saa nne usiku huku maeneo ya daraja la Nduruma Kata ya Baraa Halmashauri ya Jiji la Arusha Polisi walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne wa Ujambazi waliokutwa na bunduki moja na Bastola moja zenye jumla ya Risasi 12.

Alisema mnamo majira ya saa nne baada ya kupata taarifa fiche ambapo tuliweka mtego maeneo ya daraja la mto nduruma ndipo tulipowaona watuhumiwa hao waliotokea Dar es salaam kuja Arusha kwa kutumia gari aina ya Toyota crown, lenye namba za usajiri T. 777 DSJ ndipo walipolisimamisha gari hilo lakini walikaidi amri.

Hata hivyo askari walichukua uamuzi wa kufyatua risasi hewani kwa lengo la kuwa taadharisha lakini waliendelea kukaidi amri hiyo, ndipo askari walipoamua kufyatua risasi kwa kulenga matairi ya gari hilo hali iliyosababisha kufanikisha ukamataji wa watuhumiwa hao huku mmoja wao aitwaye Msafiri Yohana akiwa amejeruhiwa kwa risasi katika viganja vyake vya mikono.

Aidha kwa mujibu wa Kamanda Shana katika upekuzi wa gari hilo kulikutwa na aina za silaha mbili Shortgun (1) na bastola 1 zenye risasi nne za bunduki aina ya Shortgun na risasi nane za bastola zilizokuwa kwenye magazine pamoja na mikasi mitatu ya kukatia vyuma, nondo mbili, gundi na madawa mbalimbali ya mitishamba.

Alieleza Kamanda katika mahojiano na watuhumiwa hao wamekiri kuja Arusha kwa lengo la kufanya uhalifu na watuhumiwa hao watafikishwa mahakani pindi upelelezi utakapokamilika, ambapo akatoa wito kwa watu wote wenye nia ya kufanya uhalifu awatafanikiwa kuingia lakini watatoka majivu.

Pia niwaombe wananchi waendelee kutoa taarifa sahihi za uhalifu na wahalifu kwa jeshi hilo ili waweze kuzifanyia kazi hali itakayosaidia kuimarisha utulivu, amani na usalama uliyopo.

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha alilipongeza jeshi hilo kwa kufanya kazi zake kwa weledi na kuwataka wananchi kufuata maelekezo ya kutii sheria bila shuruti na wanaoshindwa mmekuwa mkiwashurutisha kama hawa.

Alisema kuwa kila wakati jeshi hilo limekuwa likiwataka wananchi kutii sheria bila shuruti na wanaokaidi mmekuwa mkiwashurutisha leo mmeonyesha mfano mmekamata majambazi wametii sheria na hawakuuwawa na matokeo yake ni tofauti na huko nyuma wengi walikuwa wakikaidi na kujikuta wakiuwawa.


No comments:

Post a Comment