ZIARA YA KATIBU MKUU, OFISI YA WAZIRI MKUU ANDREW MASSAWE AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA KIWANDA KIPYA CHA BIDHAA ZA NGOZI CHA KARANGA MKOANI KILIMANJARO - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday 26 January 2020

ZIARA YA KATIBU MKUU, OFISI YA WAZIRI MKUU ANDREW MASSAWE AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA KIWANDA KIPYA CHA BIDHAA ZA NGOZI CHA KARANGA MKOANI KILIMANJARO

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe (wa tatu kutoka kushoto) akiwa ameambatana na Viongozi kutoka Jeshi la Magereza na wasimamizi wa mradi huo alipotembelea mradi huo kwa lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho.

Mkurungenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba (wenye koti la bluu) akijadili jambo na baadhi Viongozi kutoka Jeshi la Magereza wakati wa ziara hiyo iliyofanyika Januari 25, 2020 Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe (katikati wenye koti la bluu) akizungumza na baadhi ya Viongozi kutoka Jeshi la Magereza wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho kilichopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe ametembelea eneo ambapo mradi wa ujenzi wa Kiwanda kipya cha bidhaa za ngozi cha Karanga kwa lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda hicho.
Katika ziara hiyo iliyofanyika Januari 25, 2020 Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe alikuwa ameambatana na Mkurungezi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba, PSSSF wana ubia na Jeshi la Magereza katika utekelezaji wa kiwanda hicho kilichopo Moshi, Mkoani Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment