SHIRIKA LA AFYA DUNIANI LATANGAZA CORONA KUWA JANGA LA DUNIA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Friday 31 January 2020

SHIRIKA LA AFYA DUNIANI LATANGAZA CORONA KUWA JANGA LA DUNIA




VIRUSI vipya vya corona vimetangazwa kuwa janga la dharura,wakati virusi hivyo vikiendelea kusambaa kwa kasi nje ya China, kwa mujibu wa shirika la afya duniani(WHO)

"Sababu kubwa ya tangazo hilo si kwa sababu ya kile ambacho kinatokea China kwa sasa lakini kile ambacho kinatokea katika mataifa mengine," alisema kiongozi mkuu wa shirika la afya duniani Tedros Adhanom Ghebreyesus .

Kinachoangaziwa zaidi ni kuhusu ugonjwa huo kusambaa mataifa mengine huku kukiwa na mfumo duni wa afya

Watu takribani 213 wamefariki kutokana na virusi hivyo nchini China.

Shirika la afya duniani limesema kuwa kumekuwa na visa 98 katika mataifa mengine 18 ingawa hakuna vifo vilivyobainika. Visa vingi vya wagonjwa hao walikuwa wamesafiri kutoka mji wa Wuhan, eneo ambalo mlipuko wa ugonjwa huo ulianza.

Hata hivyo kuna kesi nane zilizosababishwa na maambukizi ya kati ya mtu kwa mtu huko Ujerumani, Japan, Vietnam na Marekani.

Akizungumza katika mkutano wa habari Geneva, Dkt Tedros alielezea virusi vya corona kuwa mlipuko wa ugonjwa ambao haujawahi kutokea awali na bado haujaweza kupata suluhu.

Dkt.Tedros alisifia hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa na serikali ya China katika kuzuia maambukizi yasienee na alisema kuwa hakukuwa na sababu ya kuzuia watu wasisafiri au biashara zisiendelee.
"Lakini nataka kueleweka kuwa ,tangazo hili halimaanishi kuwa ni kura ya kutoiamini China".

Lakini nchi mbalimbali zimechukua hatua ya kufunga mipaka na kusitisha safari za ndege za nchini China, vivyo hivyo makampuni makubwa pia yamefunga maduka yao.

Itakuwaje kama virusi hivi vitasambaa katika mataifa mengine? Mataifa ambayo uchumi wake uko chini au wa katikati na ngumu kwa wao kupata vifaa vya kujizuia maambukizi au kutafuta tiba.

Hofu ipo kuwa inawezekana ugonjwa huu ushindikane kuzuilika na unaweza kumpata mtu bila kujijua wakati mwingine.

Kumbuka kuwa ugonjwa huu umeanza mwezi mmoja tu mpaka sasa na tayari kuna kesi 7,736 zimethibitishwa kuwepo nchini China na watu wakiwa wanashukiwa kuwa na ugonjwa huo.

Mwaka 2014, mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ulitokea magharibi ya Afrika, ugonjwa huo uliweka historia kubwa katika maisha ya binadamu, na ulionyesha wazi ni namna gani nchi maskini zinavyoweza kushambuliwa na mlipuko wa ugonjwa.

Na kama hali kama hii ya virusi vya ebola ingetokea katika maeneo ya aina hiyo ingekuwa ngumu sana kuzuia maambukizi.

Tuko kwenye hatua ambayo asilimia 99 ya kesi za watu wenye maambukizi iko China na shirika la afya duniani lina imani kuwa nchi hiyo inaweza kukabliana na mlipuko huo.

Lakini kutangaza kuwa janga la dharura la dunia kutaweza kuruhusu WHO kuzisaidia nchi zenye kipato kidogo na cha katikati kujiandaa kukabiliana na virusi vya corona.
-BBC

No comments:

Post a Comment