MKURUGENZI MAFIA BOXING PROMOTION ATANGAZA PAMBANO LA NGUMI KUMNADI RAIS DKT.SAMIA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday, 26 February 2025

MKURUGENZI MAFIA BOXING PROMOTION ATANGAZA PAMBANO LA NGUMI KUMNADI RAIS DKT.SAMIA

Mkurugenzi wa Mafia Boxing Promotion,  Ally Zayumba, akizungumza na waandishi wa habari Februari 25, 2025 wakati akitangaza pambano la ngumi kati ya Amir Matumla dhidi ya Paulus Amavila kutoka Namibia lenye lengo la kumnadi Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini.

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam 

MKURUGENZI wa Mafia Boxing Promotion,  Ally Zayumba amesema pambano lisilokuwa la ubingwa la Knockout ya Mama msimu wa tatu litafanyika Februari 28, mwaka huu jijini Dar es Salaam kati ya Bondia Amir Matumla dhidi ya Paulus Amavila kutoka Namibia likiwa na lengo la kutangaza kazi kubwa iliyofanywa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutekeleza miradi mbalimbali nchini.

Zayumba ameyasema hayo leo Februari 25, 2025 wakati wa mkutano na waandishi wa habari alipokuwa akitangaza mapambano hilo ambalo litakuwa la raundi nane uzito wa super weight.

“Kutokana na maandalizi mazuri tunaimani bondia wetu Matumla ambaye ni mtoto wa wa bondia wa zamani  Rashid Matumla atatuwakilisha vema kwa kufanya vizuri,” alisema Zayumba.

Zayumba alisema kuwa Amir Matumla katika pambano hilo dhidi ya MnaMIbia huyo ni pambano lake la kwanza tangu ajiunge kwenye mapambano ya ngumi za kulipwa na ambapo ametuahidi kuwa atafanya vizuri.

"Tumekaa naye tumezungumza naye na moja ya malengo yake alituambia tumtafutie pambano la kimataifa kwa hiyo litakuwa pambano lake la kwanza kwake la kimataifa," alisema.

Zayumba ameongeza kwamba siku ya pambano hilo kutakuwa na mapambano mengine 11 ya utangulizi yakiongozwa na mkongwe Dullah Mbabe, Abdallah Pazia, Oscar Richard na Yohana Mchanja   na kueleza kwamba huu ni msimu wa tatu kwa mapambano ya aina hiyo kufanyika chini ya Mafia Boxing Promotion yakiwa na lengo la kunadi miradi iliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa upande wake Amir amesema:" Nashukuru sana Mafia kwa kunipokea, naahidi Watanzania nitaendeleza kwa ukubwa zaidi, sasa hivi naendelea na mazoezi, watu waje kwa wingi watafurahi zaidi

 Zayumba alitaja viingilio katika pambano hilo kuwa ni Sh. 50,000, 20,000 na sh 10,000.

No comments:

Post a Comment