RC WANGABO NA ZIARA YENYE CHANGAMOTO, ALAZIMIKA KUACHA GARI…! - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday 2 March 2019

RC WANGABO NA ZIARA YENYE CHANGAMOTO, ALAZIMIKA KUACHA GARI…!

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (mbele) akivuka daraja la miti lililojengwa juu ya mto Kalambo kuelekea katika kitongoji cha Kamleshe ambacho kipo karibu na Kijiji cha Jengeni alipokwama kuendelea na safari kwa siku ya kwanza.  

 Gari la Mkuu wa Wilaya ya Kalambo likiwa limekwama na kujaribu kukwamuliwa kutoka kwenye tope zito liliosababishwa na mvua zilizonyesha hivi karibuni na kusababisha hali ya barabara kuwa mbaya. 

Gari waliopanda wataalamu kutoka Ofisi ya mkoa wa Rukwa likiwa limekwama huku wataalamu hao kwa ushirikiano na wajumbe wa Kamati ya ulinzi ya Mkoa wakijaribu kulikwamua kutoka kwenye tope zito wakati wakitokea kijiji cha Jengeni Kata ya Kitete, Wilayani Kalambo. 

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Julieth Binyura akivuka daraja la miti kuelekea katika kijiji cha Jengeni, Kata ya Kitete, Wilayani Kalambo. daraja hilo ndilo wanalotumia wananchi katika shughuli zao za kila siku hasa wakati wa masika. Chini ya daraja hilo unapita mto China.

Kaimu katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Albinus Mgonya akivuka daraja la miti kuelekea katika kijiji cha Jengeni. kuonana na wananchi kisha kuelekea katika kitongoji cha Kamleshe kilichopo kijiji cha Nondo, Kata ya Mpombwe, Wilayani Kalambo.  

No comments:

Post a Comment