MWANAMAZINGIRA AJITOSA KUWANIA UDIWANI KATA YA LIGOMA TUNDURU - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Thursday, 26 June 2025

MWANAMAZINGIRA AJITOSA KUWANIA UDIWANI KATA YA LIGOMA TUNDURU

Mtia nia nafasi ya Udiwani Kata ya Ligoma Tunduru Ruvuma, Shukuru Shahibu Selemani.

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

KIJANA na mdau wa mazingira Shukuru Shahibu Selemani (35) ametangaza nia ya kugombea Udiwani Kata ya Ligoma Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma kupitia Chama Cha Mapinzuzi (CCM), ili kupambana na Diwani aliyemaliza muda wake,  Abdallah Zuberi Mmara ambaye ametangaza kutetea nafasi hiyo.

Wagombea wengine ambao wanatajwa kuwania nafasi hiyo ni Ahusi Manganya, Juma Jasi na Daud Likwata wote wakiwa wakazi wa kata hiyo ya Ligoma.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Juni 25, 2025, Shukuru alisema ameonesha nia ya kugombea nafasi hiyo kwa lengo la kuchochea maendeleo zaidi kwenye kata hiyo kutokana na kuwa na uwezo.

“Ni ukweli usiopingika kwamba Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya maendeleo makubwa katika kata yetu tunamshukuru sana mama yetu na nimeamua kugombea nafasi hii ili kuongeza kasi  ya maendelea kuanzia pale alipoichia diwani aliyemaliza muda wake ndugu Abdallah Mmara,” alisema Shukuru.

Shukuru alisema anagombea nafasi hiyo kupitia CCM kwa mara ya pili na awamu ya kwanza aligombea kupitia Chama cha Wananchi CUF kabla ya kuhamia chama tawala.

Alisema kwa mara ya kwanza kugombea nafasi hiyo kuptia CCM katika mchakato wa kura za maoni  hazikutosha ambapo alishika nafasi ya pili akiongoza diwani ambaye amemaliza muda wake hatua ambayo inampa matumaini makubwa ya kushinda  awamu hii.

Shukuru Shahibu Selemani ni mtaalamu wa usafi wa mazingira mwenye taasisi inayotoa mafunzo na kuhamasisha utunzaji wa mazingira  katika shule mbalimbali nchini.

Pamoja na kujishughulisha na kazi hiyo pia anajishughulisha na uchimbaji mdogo wa madini ambapo anashirikiana na vijana kutoka maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Tunduru hasa katika kata hiyo akiwa kiongozi wao.

No comments:

Post a Comment