MAMA AWAOMBA WATANZANIA KUSAIDIA MATIBABU YA MTOTO WAKE ANAYETESEKA KWA MARADHI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday, 24 May 2025

MAMA AWAOMBA WATANZANIA KUSAIDIA MATIBABU YA MTOTO WAKE ANAYETESEKA KWA MARADHI

Mtoto Abubakar Tenda (10) anayesumbuliwa na maradhi ya pumu ya ngozi na moyo kwa zaidi ya miaka tisa.


Na Dotto Mwaibale


LATIFA Saidi (37) mkazi wa Mtoni Mtongani Mtaa wa Mseti Temeke Jijini Dar es Salaam anawaomba wadau mbalimbali kumsadia kupata  Sh. Milioni 3.2 kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake Abubakar Rajabu Tenda (10) anayesumbuliwa na maradhi ya pumu ya ngozi na moyo kwa zaidi ya miaka tisa.


Mama huyo anasema alimzaa Abubakar Juni 10, 2014 Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Temeke Jijini Dar es Salaam akiwa na kilo 4.5 jambo ambalo liliwashitua hata wauguzi waliokuwa wakimuhudumia.


Anasema alianza kuona mabadiliko ya mtoto huyo alipofikisha miaka mitatu kwani ngozi yake ilianza kuonesha kutokwa na upele ndipo alipo mpeleka Hospitali ya kwa Bruda iliyopo Kijijichi lakini hakupata nafuu.


Latifa anasema aliendelea kumtibu katika hospitali mbalimbali na alipofikisha miaka sita akawa anapata joto kali nyakati za usiku, kukooa sana na uso kuvimba ndipo alipompeleka tena Hospitali ya Temekea ambapo walimuambia kuwa alikuwa na changamoto ya moyo hivyo ampeleke Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa ajili ya matibabu.


Alisema baada ya kufanyiwa vipimo alielezwa kuwa moyo wake umetanuka hivyo anatakiwa kufanyiwa upasuaji kwa gharama ya fedha Sh. Milioni 3.2 fedha ambazo ameshindwa kuzipata jambo linalomfanya mtoto wake huyo aendelee kuteseka na kushindwa kuanza shule.


“Kwa kweli sijui hatima ya mwanangu kwani wakati wote hana furaha na sijui nitapata wapi hizo fedha sina kazi zaidi ya kuuza vijiazi hapo epenuni kwa nyumba ya jirani na mume wangu naye hana kazi ya uhakika hivyo kutuwia vigumu namna ya kupata fedha hizo,” alisema Latifa.


Alisema mwezi uliopita ndio ilikuwa ampeleke kliniki lakini hadi leo hii ameshindwa kufanya hivyo kwani kila inapofika tarehe ya kliniki anatakiwa awe na Sh. 120,000 kwa ajili ya vipimo na mahitaji mengine ya chakula, na usafiri fedha ambayo hana kwani hatakodi ya nyumba ambayo ni zaidi ya Sh.250,000 ameshindwa kulipa.


“Kwa kweli sina mbele wala nyuma sijui nitazimaliza vipi hizi changamoto nilizonazo nawaombeni watanzania wenzangu kwa nafasi zenu mlizojaaliwa na Mwenyezi Mungu mnisaidie hasa fedha na matibabu ya mtoto wangu ambaye anapenda kusoma lakini ndio hivyo tena maradhi yanamsumbua,” alisema Latifa huku akitokwa na machozi na kuonesha kukata tamaa.


Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Mianzini Maji Matitu 'A' Mbagala kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hawa Omari ambaye amemuibua mtoto huyo ameiomba jamii na watanzania kwa ujumla kuungana kwa kufanya vitendo vya huruma kwa makundi mbalimbali ya wenye uhitaji na changamoto za aina tofautitofauti jambo litakalosaidia kuwa na taifa lenye upendo badala ya kusubiri mambo hayo kufanywa na Serikali.


Ndugu zangu watanzania Latifa Saidi anaomba msaada wetu kwa chochote kile atakachosaidiwa kwake kitakuwa ni kikubwa kwa yeyote atakaye guswa na kutaka kumsaidia ana weza kuwasiliana naye moja kwa moja kwa namba ya simu 0788034472 au Mwandishi wa taarifa hii kwa namba 0754362990.

Mtoto Abubakar Tenda (10) anayesumbuliwa na maradhi.
Mtoto Abubakar Tenda (10) akiwa na mama yake.
Mtoto Abubakar Tenda (10) anayesumbuliwa na maradhi akiwa amekaa na mama yake nje ya upenu wa nyumba ya jirani yao anapojishughulisha mama huyo kutengeneza sambusa za viazi mviringo ili aweze kujipatia fedha za kujikimu katika maisha ya kila siku.
 

No comments:

Post a Comment