RAIS SAMIA AWAAPISHA MABALOZI, IKULU CHAMWINO, DODOMA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 16 August 2023

RAIS SAMIA AWAAPISHA MABALOZI, IKULU CHAMWINO, DODOMA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi, Mabalozi Wateule pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya Uapisho iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.

Mabalozi Wateule wakisaini Hati za kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.

Mabalozi Wateule wakila Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.

Mabalozi Wateule wakila Kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Hassani Iddi Mwamweta kuwa Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Meja Jenerali Paul Kisesa Simuli, kuwa Balozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Habibu Awesi Mohamed kuwa Balozi wa Tanzania nchini Qatar kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Bw. Iman Salum Njalikai, kuwa Balozi wa Tanzania nchini Algeria kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 16 Agosti, 2023.





No comments:

Post a Comment