NMB, ATCL ZAZINDUA USHIRIKIANO, WASAFIRI KULIPIWA BIMA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 16 August 2023

NMB, ATCL ZAZINDUA USHIRIKIANO, WASAFIRI KULIPIWA BIMA

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipunda (wa pili kulia) pamoja na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mhandisi Ladislaus Matindi (wa pili kulia) wakiwa wameshikilia mfano wa ndege za ATCL mara baada ya kuzinduwa mfumo wa malipo ya tiketi, ambapo msafiri wa ATCL atakayelipia kupitia tiketi yake kupitia matawi na mawakala wa benki hiyo atanufaika na Bima ya Safari moja kwa moja.

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipunda (wa pili kulia) pamoja na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mhandisi Ladislaus Matindi (wa pili kulia) wakiwa wameshikilia mfano wa ndege za ATCL mara baada ya kuzinduwa mfumo wa malipo ya tiketi, ambapo msafiri wa ATCL atakayelipia kupitia tiketi yake kupitia matawi na mawakala wa benki hiyo atanufaika na Bima ya Safari moja kwa moja.

NA MWANDISHI WETU

BENKI ya NMB na Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wamezindua ushirikiano wa kibiashara wa mifumo ya malipo ya tiketi za ndege 'Anga Rafiki - Tiketi Yako Imebima,' unaowapa fursa wasafiri wa Shirika hilo kulipia tiketi kupitia matawi, mawakala na huduma za NMB Mkononi na NMB App, ambazo zitakuwa zimekatiwa Bima ya Safari moja kwa moja.

Ushirikiano huo umezinduliwa Makao Makuu ya NMB jijini Dar es Salaam leo Jumatano Agosti 16, ambako msafiri atakayelipia tiketi za safari za ndani na nje ya nchi kupitia NMB, atakatiwa bima ya maisha, ulemavu ama upotevu wa mizigo safarini, ambapo atalipwa hadi Sh. Mil. 5 za Kitanzania itapotokea mteja kufariki dunia.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), Ruth Zaipuna, alisema kwamba, kupitia matawi 229 na mawakala zaidi ya 21,000, wasafiri nchini wanaenda kufikiwa kirahisi kuwezesha upataji tiketi na kwa wateja wa benki hiyo wanazo njia za ziada za kulipia tiketi hizo kwa simu ya mkononi kupitia USSD na NMB App.

"Ni imani yetu sisi NMB kwamba, huduma hii sio tu inaenda kumpa urahisi na wepesi msafiri wa kulipia tiketi yake, bali kumkinga pia na majanga yatokanayo na safari kama ulemavu, kifo na upotevu wa mizigo.

"Mteja akilipia tiketi ya ATCL kupitia NMB, ikatokea akafariki - ingawa hatuliombei hilo, ama kupata ulemavu akiwa safarini, yeye ama wategemezi wake watalipwa hadi Sh. Milioni 5.

"Na iwapo mzigo (checked in Baggage) wa msafiri utapotea, mteja wetu atalipwa Shilingi 300,000, lakini pia ikiwa safari itasogezwa ama kuahirishwa, atalipwa Shilingi 150,000. Bima hizi tutazilipa kupitia washirika wetu Kampuni ya Reliance Insurance," alifafanua Zaipuna.

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipunda (wa pili kulia) pamoja na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mhandisi Ladislaus Matindi (wa pili kushoto) wakipongezana mara baada ya kuzinduwa mfumo wa malipo ya tiketi, ambapo msafiri wa ATCL atakayelipia kupitia tiketi yake kupitia matawi na mawakala wa benki hiyo atanufaika na Bima ya Safari moja kwa moja.

Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Bi. Ruth Zaipunda (wa pili kulia) akizungumza kwenye uzinduzi huo wa mfumo wa malipo ya tiketi, ambapo msafiri wa ATCL atakayelipia kupitia tiketi yake kupitia matawi na mawakala wa benki hiyo atanufaika na Bima ya Safari moja kwa moja.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, Ladislaus Matindi, aliipongeza NMB sio tu kwa ushirikiano wao huo, bali kuweka ziada ya Bima ya Safari kwa wateja wao, huku akibainisha kwamba hakuna tena sababu ya Watanzania kusafiri kwa hofu wakati kuna ATCL na NMB.

"ATCL kila siku tumejikita katika kuboresha utoaji huduma zetu, kuanzia tiketi inapokatwa, mteja anapokuwa safarini hadi kufika, hivyo tunajivunia ushirikiano wetu na NMB, ambao unaenda kututofautisha na watoa huduma za usafiri wa anga wengine waliopo sokoni.

"Ni ushirikiano unaoenda kumaliza kabisa hofu ya upatikanaji tiketi za safari na usalama wa abiria wetu na mali zao wawapo safarini, hii ni kutokana na ziada zilizowekwa na NMB kwa abiria watakaolipia kupitia mtandao wao mpana wa matawi, mawakala na huduma za NMB Mkononi kama alivyotangulia kusema CEO Zaipuna," aliongeza Matindi.

Matindi alienda mbali zaidi na kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kila aina ya uwezeshaji inaowapa katika kutoa huduma kwenye Sekta ya Usafiri wa Anga kitaifa na kimataifa, ambako kufikia mapema mwakani watatanua mtandao wa ndege zao kufikia 16.

Aliitaka NMB kujiweka tayari kuhudumia wateja wa ndege zao hizo, ikiwamo kujenga mazingira ya kuongeza chachu ya usafirishaji wa mazao na bidhaa za ndani kwenda nje ya nchi, huku akimaliza kwa kuhoji kwanini abiria wasafiri kwa hofu wakati kuna ushirikiano chanya mfano wa huo wa Shirika lake na benki hiyo.

No comments:

Post a Comment