SEKTA YA UTANGAZAJI YA HIMIZWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Thursday 29 July 2021

SEKTA YA UTANGAZAJI YA HIMIZWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI


Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Jabiri K. Bakari akizungumza NA Washiriki katika Mkutano wa Madau, Maudhui ya Utangazaji-Jijini Dodoma.



Washiriki katika Mkutano wa Madau, Maudhui ya Utangazaji. 

SERIKALI imehimiza watoa huduma za Mawasiliano Nchini, kuzingatia Sheria na Kanuni zilizomo kwenye Leseni katika Utoaji wa huduma husika kwa Wananchi.

Akizindua kikao cha Watoa Huduma za Utangazaji na Maudhui Jijini Dodoma Tarehe 28-07-2021, wadau kutoka Azam Media, Multchoice Tanzania limited, Watoa Huduma kwa njia ya Cable, COSOTA na TFF ni baadhi ya washiriki waliohudhuria ambapo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri K. Bakari, amesema baadhi Kanuni za Maidhui na Utangazaji zinafanyiwa maboresho na zinatarajia kuanza hivi karibuni

Dkt. Jabiri amesema kuwa TCRA imeboresha utendaji kazi zake kwa kuweka mifumo madhubuti zaidi na imeendelea kutoa ushauri kwa watoa huduma kila mara. Kikao hichoshirikishi pia kilihudhuliwa na watoa huduma za utangazaji na maudhui kutoka vyombo vya habari mbalimbali.

Kikao hicho ambacho kimeratibiwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kanda ya kati, kililenga kutoa elimu ya namna bora zaidi katikakufikisha maudhui kwa walaji bila kuwa na migongano baina ya watoa huduma. Pia kikao kimependekeza wanaochakata maudhui kuangalia namna nzuri zaidi ya kuzuia maudhui yasiyo na staha kwa Jamii ili kuondoa malalamiko ndani yaJamii.

Kikao kimependekeza pia vikao kama hivi viwe vinafanywa mara kwa mara ili kuongeza ufahamu zaidi kwa watoa huduma na Mamlaka za Serikali zinazosimamia sekta ya maudhui ya Utangazaji.

 

No comments:

Post a Comment