TIMU YAUNDWA UTATUZI MIGOGORO YA ARDHI NYAKASANGWE MANISPAA YA KINONDONI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 19 August 2020

TIMU YAUNDWA UTATUZI MIGOGORO YA ARDHI NYAKASANGWE MANISPAA YA KINONDONI

Waziri wa Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi , Mhe. Willium Lukuvi katikati akiwasikiliza wananchi wa Nyakasangwe Kata ya Wazo wakati alipofanyao mkutano kwa ajili ya utatuzi wa mgogoro wa Adhi unaowakabili wananchi hao.kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo akiwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Ndug. Aron Kagurumjuli pamoja na Mkuu wa Idara ya Ardhi Maduhu Kazi.


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo akizungumza na Wananchi wa Nyakasangwe Kata ya Wazo wakati wa kikao cha utatuzi wa migogoro ya Ardhi.

WIZARA ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kushirikiana na Manispaa ya Kinondoni imefanikiwa kutatua changamoto ya mgogoro wa Ardhi uliodumu kwa kipindi cha miaka saba katika eneo la Nyakasangwe Kata ya Wazo kwa kuunda timu itakayofanya tathimini kwa awamu ya mwisho.

 Akizungumza na Wananchi wa eneo hilo, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Wilium Lukuvi amesema kuwa mgogoro huo unaohusisha eneo lenye takribani ekari 2878, umegawanyika katika  makundi mawili ambayo ni upande wa wenyemashamba pamoja na wenye makazi  wanaokadiriwa  kufikia idadi ya watu  3300.

“Nimepokea taarifa ya watalamu wangu lakini bado kunamapangufu kiasi, hivyo nimekuja na timu nyingine kutoka makao makuu ya Jeshi la Polisi Dodoma ambao watafanya kazi kwakushirikiana na Manispaa ya Kinondoni watafika huku muwape ushirikiano, kama mtu ulinunua eneo kwa mtu basi uwe na nyaraka zako” amesema Mhe. Lukuvi

Ameongeza kuwa timu hiyo itaanza kufanya utambuzi kutokana na ripoti ya timu ya awali iliyoundwa na kwamba iwapo itabaini kunauvamizi ulifanyika kwa wanchi hao, serikali haitawavunjia nyumba badala yake watapaswa kulipia gharama ya eneo hilo sambamba na mwenyemashamaba halali na nyumba halali .

Awali akimkaribisha Mhe. Waziri Lukuvi, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo alisema kuwa kwasasa Manispaa ya Kinondoni imefanikiwa kupima viwanja takriban 9000, hali iliyopelekea kupunguza migogoro hiyo kwa kiasi kikubwa na hivyo kumpongeza Mkurugenzi wa Manispaa Kagurumjuli kwa usimamizi mzuri wa Ardhi.

Mhe. Chongolo amesema Wananchi ambao tayari wameshapimiwa viwanja vyao wanapaswa kuchukua hati zao sambamba na wale ambao maeneo yao hajapimwa kuchukua hatua ili kuepukana na usumbufu wowote unaoweza kujitokeza.

No comments:

Post a Comment