DK MAGUFULI ATOA BILIONI 78 KUDHIBITI SUMUKUVU – KATIBU MKUU KUSAYA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Friday, 31 July 2020

DK MAGUFULI ATOA BILIONI 78 KUDHIBITI SUMUKUVU – KATIBU MKUU KUSAYA

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya akipokea maelezo kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Itilima, mkoani Simiyu, Mhe. Benson Kilagi mara baada ya kufika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya leo tarehe 31 Julai, 2020.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya mara baada ya kufika kwenye Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima leo tarehe 31 Julai, 2020.

Katibu Mkuu Kilimo Bwana Gerald Kusaya akipokea taarifa ya maendelo ya Sekta ya Kilimo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, Bibi Elizabeth Gumbo.

SERIKALI ya Rais, Dkt. John Pombe Magufuli imetoa kiasi cha Dola za Marekani milioni 35.3 sawa na bilioni 78 fedha Kitanzania kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Kudhibiti Sumukuvu nchini (Tanzania Prevention for Afflatoxin Contamination - TANPAC). 
Sumukuvu inatokana na fangasi wanaoota kwenye mazao ya chakula hususan mahindi na karanga, ambapo fedha hizo zitatumika kujenga miundombinu mbalimbali, ikiwemo maghala katika Halmashauri 14 Tanzania Bara na Zanzibar.
Akizungumza kabla ya kutembelea eneo litakalojengwa ghala la kuhifadhia mazao ya chakula katika kijijini cha Ikindilo wilayani Itilima mkoani Simiyu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bwana Gerald Kusaya anasema fedha hizo zitatumika kujenga maabara mahususi ya kilimo Jijini, Dodoma; Kituo cha karantini ya utafiti wa Sumukuvu, Kibaha mkoani Pwani pamoja na Kituo mahili cha mazao eneo la Mtanana, mkoani Dodoma.
Aidha, Katibu Mkuu Kusaya amesema kupitia mradi wa TANPAC Serikali itajenga Maghala 14 kwa ajili ya kuhifadhi mazao ya chakula aina ya nafaka na kutumia fursa hiyo kuziomba Halmashauri hizo 12 (Tanzania Bara) na mbili Zanzibar kutoa maeneo ambayo hayatakuwa na migogoro ya ardhi ili maghala hayo yajengwe mara moja.
Katibu Mkuu Kusaya ameongeza kuwa thamani ya kila ghala, litakalojengwa katika Halmashuri kila Halmashauri; Litagharimu kiasi cha shilingi milioni 480 na kuongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kumkomboa Mkulima kutokana na changamoto ya sumukuvu ambayo ina athari kubwa kwa afya za walaji pamoja na biashara ya mazao ya kilimo ndani na nje ya nchi.

“Nawaomba Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya, Wakulima na Wananchi ambao Halmashauri zao zimepata fursa ya kujengewa maghala haya, waridhie na wataoe maeneo ambayo hayana migogoro ili mwezi Disemba, 2020 tuanze ujenzi, fedha ipo tayari na mchakato wa kuwapata Wazabuni upo kwenye hatua ya mwisho.” Amekaririwa Katibu Mkuu Kilimo, Bwana Gerald Kusaya.

No comments:

Post a Comment