WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA INNOCENT BASHUNGWA ATEMBELEA KIWANDA CHA MWATEX MWANZA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 11 December 2019

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA INNOCENT BASHUNGWA ATEMBELEA KIWANDA CHA MWATEX MWANZA


Mhe. Innocent Bashungwa Waziri wa Viwanda na Biashara akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoa Mwanza amekitembelea kwa mara ya pili kiwanda cha Mwatex (2001) LTD kilichobinafisiswa na Serikali kwa mwekezaji Amin Radhanin na chenye wafanyakazi 600.
Kwenye ziara ya kwanza ya tarehe 30/09/2019 alitoa maelekezo kwa kiwanda kuhusu kuandaa mpango mkakati wa biashara wa kuendesha kiwanda lakini mpaka sasa huo mpango mkakati haujafika wizarani.

Waziri baada ya kufika kiwandani hapo aliomba uongozi na menejiment nzima kutoka nje na mkutano ili kusikiliza kero na changamoto pia na maoni yao yatakayofanya kiwanda hicho kinafanye kazi kwa asilimia 100.

Amabapo kwa sasa kinafanya kazi asilimia 60 tofauti na matalajio ya serikali ya kiwanda kufanya kazi kwa asilimia 100 Waziri baada ya kusikiliza maona na kero za wafanyakazi ameagiza wizara kuunda kamati maalum ambayo itafika kiwandani kufanya uchambuzi wa uendeshaji wa kiwanda kwa kushirikiana na msimazi anaekiendesha kiwanda hicho na amewapa muda mpaka 01/01/2020 kamati hiyo iwe imeshamfikishia ripoti ya uchambuzi wa mwenendo wa kiwanda cha Mwatex Ripoti hiyo itaisaidia serikali kupata mwelekeo wa nini kifanyike ili kupata Mwatex iliyokuwepo enzi za Mwalimu Nyerere.

Pia Waziri amesisitiza kuwa mkakati wa serikali ni kuona viwanda vyote vinafufuliwa na vinafanya kazi ili serikali iweze kutengeneza mnyororo wa thamani ya mazao yote hapa nchini.

No comments:

Post a Comment