NAPE AMUOMBA MSAMAHA RAIS MAGUFULI IKULU…! - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday, 11 September 2019

NAPE AMUOMBA MSAMAHA RAIS MAGUFULI IKULU…!

Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM), Nape Moses Nnauye akiwa Ikulu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli alipokwenda kumuomba msamaha kwa kumkosea.



Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM), Nape Moses Nnauye akiwa Ikulu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli alipokwenda kumuomba msamaha kwa kumkosea.

Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM), Nape Moses Nnauye akiwa Ikulu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli alipokwenda kumuomba msamaha kwa kumkosea.

NAPE AMUOMBA MSAMAHA RAIS MAGUFULI IKULU…!

MBUNGE wa Jimbo la Mtama (CCM), Nape Moses Nnauye leo amefika Ikulu na kuomba msamaha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli kwa yote aliyomkosea. Hata hivyo Rais Magufuli ametangaza kumsamehe mbunge huyo machachari wa CCM na kumtaka aendelee kuchapa kazi kwa kuwatumikia watanzania katika nafasi alizonazo.

Akizungumza Ikulu mara baada ya mazungumzo na mbunge Nape, Rais Dk Magufuli alisema amekuwa akipokea ujumbe mfupi mara kadhaa wa mbunge huyo akiomba kusamehewa kwa popote alipoteleza.

Aidha Rais Magufuli amesema amemsamehe kwa moyo mweupe kwa kuwa yeye kama binadamu wengine wamefundishwa kusamehe kiimani, hivyo hawezi kuendelea kuweka kinyongo moyoni hata kama alimkosea.

Nape sasa anaingia kwenye orodha ya wanasiasa wenzake vijana, yaani January Makamba na William Ngeleja ambao nao waliamua kujirudi na kumuomba msamaha rais kwa makosa waliomkosea, ambao nao Rais Magufuli alitangaza kuwasamehe kwa moyo mweupe.

No comments:

Post a Comment