JE, WAJUA PROGRAM YA 'WHAT3WORDS' INAWEZA KUOKOA MAISHA YAKO - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 19 August 2019

JE, WAJUA PROGRAM YA 'WHAT3WORDS' INAWEZA KUOKOA MAISHA YAKO

Programu tumishi ya "What3words" imegawa dunia katika pande trilioni 57 na kila upande ukiwa na anuani ya kipekee ya maneno matatu.
PROGRAMU tumishi ya "What3words" imegawa dunia katika pande trilioni 57 na kila upande ukiwa na anuani ya kipekee ya maneno matatu. Polisi nchini Uingereza wametaka kila mtu kupakuwa programu tumishi ya simu ya mkononi wakidai kuwa programu hiyo imeshaokoa baadhi ya maisha ya watu. Je programu hiyo ni ipi na inafanya kazi vipi? 'Kicked. Converged. Soccer' yaani Imepigwa, Imegeuzwa, Soka.

Maneno hayo matatu ambayo yamechaguliwa bila kuwa na mpangilio yaliweza kuokoa maisha ya Jess Tinsley na rafiki zake baada ya kupotea kwenye msitu usiku. Nilipopiga simu ya dharura jambo nililoambiwa kufanya ni kupakua programu ya 'what3words', nilikuwa sijawahi kuisikia kabla, baada ya dakika chache, polisi walijibu kwa kutuuliza ni wapi tulipo,"Bi.Tinsley alisema.

"Nilimwambia kila mtu ninayemjua kupakua programu hii kwa sababu hawawezi jua lini wanaweza kupotea na kuhitaji huduma hiyo,"Bi. Tinsley aliongeza.

Wavumbuzi wa programu hiyo ndio waliigawa dunia katika pande trilioni 57 kwa mita 3 na kila upande kuna maneno matatu ambayo hayana mpangilio kuainisha anuani ya sehemu husika.

Programu hii ilianza kutumika na muasisi wa kampuni hiyo Chris Sheldrick ambaye alipata changamoto hizo kwa kuwa alikuwa anaishi katika maeneo ya vijijini huko Hertfordshire, Uingereza.

"Tulikuwa tunapata barua za watu wengine katika nyumba yetu kwa sababu nyumba yetu ilikuwa haina anuani". Miaka 10 akiwa tasnia ya muziki ambayo alipata changamoto kubwa ya kuwasiliana na bendi mbalimbali kufika katika ukumbi, ilimlazimu kutafuta suluhu la tatizo linalomkabili.

"Nilijaribu njia mbalimbali za kufika eneo niliko bila mafanikio, hivyo ikanifanya niwaze zaidi njia ambayo ni rafiki", Shedrack alieleza.

Kampuni ya programu tumishi hiyo ilianza mwaka 2013 na sasa imewaajiri watu zaidi ya 10o kaskazini mwa mji wa London.

"Kama watu hawana programu tumishi hiyo, huduma ya dharura inaweza kutuma ujumbe mfupi unaojumuisha anuani ya tovuti hiyo katika simu zao.

Lakini Programu tumishi inahitaji mtandao wa intanet ingawa haiitaji mtu kuwa na mtandao wa simu kusema maneno hayo matatu ya kujulisha eneo la mtu alipo", bwana Sheldrick alisema.

"Hata kama hamna mtandao bado mtu anaweza kusaidiwa kama atajua maneno matatu ya eneo husika".

Watu waliokolewa kupitia progamu hiyo inawafanya waasisi wa programu hiyo kuwa wamefanya kazi ya maana.
-BBC

No comments:

Post a Comment