WAZIRI MKUU MAJALIWA AISIFIA BENKI YA NMB...! - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Monday 24 June 2019

WAZIRI MKUU MAJALIWA AISIFIA BENKI YA NMB...!

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya soka ya Bunge, Cosato Chumi baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa 5-3 dhidi ya timu ya NMB katika Bonanza la Benki ya NMB na Wabunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya Mpira wa Kikapu ya Benki ya NMB – Danford Kisinda baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa vikapu 54-52 dhidi ya timu ya mpira wa Kikapu ya Bunge katika mechi ya Bonanza la Benki ya NMB na Wabunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania – Tulia Ackson na Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB wakiwa pamoja na timu ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wakifurahia ushindi wa timu za bunge kwenye Bonanza la michezo la NMB na Bunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

Kaimu Mkurugenzi wa Benki ya NMB akishangilia ushindi wa Mpira wa Kikapu baada ya kuwashinda timu ya Bunge kwa Vikapu 54 kwa 52 kwenye Bonanza la michezo la NMB na Bunge lililofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma mwishoni mwa juma.

No comments:

Post a Comment