OFISI YA WAZIRI MKUU YAHAMIA RASMI MJI WA SERIKALI, DODOMA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Tuesday 16 April 2019

OFISI YA WAZIRI MKUU YAHAMIA RASMI MJI WA SERIKALI, DODOMA

Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akiwa anatekeleza majukumu yake katika Ofisi yake Mpya iliyopo katika Mji wa Serikali Kata ya Mtumba, Jijini Dodoma ikiwa ni kutekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alilotoa tarehe 13 Aprili, 2019.

Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akizungumza na baadhi Wakuu wa Idara na Vitengo wakati alipofanya kikao cha kuwakaribisha katika ofisi zao mpya zilizopo katika Mji wa Serikali Aprili 15, 2019.

Katibu Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge) Bi. Maimuna Tarishi akiwaonesha baadhi ya Watumishi wa Ofisi yake (hawapo pichani) namna Mji wa Serikali ulivyo walipofanya ziara ya kuzunguka kujua maeneo mbalimbali ya Wizara na huduma zilizopo katika Mji huo.

No comments:

Post a Comment