WAZAZI WATAKIWA KUTOWAFICHA WATOTO WENYE UWALEMAVU - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday, 7 May 2025

WAZAZI WATAKIWA KUTOWAFICHA WATOTO WENYE UWALEMAVU

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Bw. Greyson Mgoi (kulia) akizungumza na wazazi kwenye ziara za washiriki wa Juma la Elimu kutembelea shule mbalimbali wilayani Mpimbwe Mkoa wa Katavi.

Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu kwenye ziara za wadau wa elimu kutembelea shule anuai na kuzungumza na wazazi, viongozi na wadau wengine wa elimu.

Mratibu Taifa wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Bi. Martha Makala akifurahi na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi kwenye ziara za wadau wa elimu kutembelea shule na kuzungumza na wazazi, viongozi na wadau wengine wa elimu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Juma la Elimu Kitaifa (GAWE) 2025, Bw. Greyson Mgoi (kulia) akizungumza na wazazi kwenye ziara za washiriki wa Juma la Elimu kutembelea shule mbalimbali wilayani Mpimbwe Mkoa wa Katavi.

Wanafunzi wakishangilia kwenye moja ya mikutano ya sehemu ya Maadhimisho ya Jumala la Elimu Kitaifa, mkoani Katavi.

Sehemu ya wazazi wakiwa katika mikutano na washiriki wa Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025, kwenye ziara katika shule mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Mpimbwe, mkoani Katavi, ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu (GAWE) 2025.

Sehemu ya Wanachama wa Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), na wadau wengine wa elimu wakiwa katika moja ya ziara kutembelea shule na kuzungumza na wazazi, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho.

WAZAZI wilayani Mpimbwe Mkoa wa Katavi  wametakiwa kutowaficha watoto wenye ulemavu nyumbani na badala yake  watoe taarifa kwa viongozi wa vijiji na na shule ili watoto hao waweze kupewa nafasi ya kupata Elimu. 

Akizungumza na Kundi la Wazazi leo katika Kijiji Cha Mbede, wilayani Mpimbwe, wakati wa Ziara za kutembelea Shule za Maadhimisho ya Juma la Elimu, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Maazimisho hayo Kitaifa, Bw. Greyson Mgoi, alisema hakuna sababu yeyote ya kuwaficha watoto wenye ulemavu nyumbani kwa kuwa nao wanayo haki ya kupata elimu bora itakayowasaidia katika maisha yao ya badae. 

Bw. Mgoi ambaye pia ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Habari na Uchechemuzi wa Shirika la Uwezo Tanzania, alisema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatekeleza Sera ya Elimu bila malipo kwa watoto wote hivyo, si sahihi kwa wazazi wenye watoto wenye ulemavu kuwaficha ndani.

"Watoto wenye ulemavu wanayo haki ya kupata Elimu, tusiwanyime haki yao ya msingi, kama unaye mtoto mwenye ulemavu toa taarifa kwa viongozi katika eneo lako au fika shuleni itoe taarifa kwa mwalimu mkuu, utaweza kumsaidia mtoto huyo kupata elimu.

Serikali pamoja na wadau mbalimbali wanafanya jitihada kubwa za kuhakikisha kundi hili nalo linapata elimu bora," alisema Bw. Mgoi.

Sambamba na hilo, Mgoi alisema kuwa Wazazi wanapaswa kuwasaidia watoto wote kukuza stadi za ujuzi mbalimbali suala ambalo ni muhimu kwa maisha yao.

Kauli mbinu ya mwaka huu ya Maadhimisho ya Juma la Elimu ni Elimu na Ujuzi kwa Maendelea ya Taifa, ambayo inapaswa kutekelezwa kwa vitendo na wadau wote wakiwemo Wazazi ili kuboresha Elimu ya wototo wote.

Maadhimisho ya Juma la Elimu yalizinduliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mh. Mwanamvua Mrindoko Mei 5, 2025 Katika Kata ya Majimoto, Wilaya ya Mpimbwe, mkoani Katavi na yanatarajiwa kuhitimishwa Mei 9, 2025. 

Wadau kutoka katika zaidi ya mashirika yasiyo ya kiserikali 50 yanashiriki kwenye maadhimisho hayo ya Kitaifa, likiwemo Shirika la Uwezo Tanzania.

No comments:

Post a Comment