WABUNGE WAPONGEZA SERIKALI MRADI WA SOKO LA KARIAKOO - THE HABARII
.com/img/a/
ASAS GROUP
.com/img/a/

Monday, 14 April 2025

demo-image

WABUNGE WAPONGEZA SERIKALI MRADI WA SOKO LA KARIAKOO

KMC%202
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Festo Dugange (wa kwanza kulia) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila wakati wa ukaguzi wa mradi wa Soko la Kariakoo leo Aprili 12,2025 ambapo amesema mradi huo umekamilika kwa asilimia 98 na kuwa soko hilo litafanya kazi kwa saa 24 za siku.

KMC%206
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Justin Nyamoga akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara ya ukaguzi wa Soko la Kariakoo katika ukumbi wa Arnatouglo leo Aprili 12, 2025 Dar es Salaam ambapo ameshauri Serikali kuhakikisha wafanyabiashara wote wenye sifa wanarejeshwa kwa haki na usawa ili kuepusha malalamiko. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila.

KMC%207
Mwonekano wa juu wa Soko jipya la Kariakoo leo wakati Kamati ya Bunge ya TAMISEMI ilipokagua utekelezaji wa mradi huo ambapo imeridhishwa na jinsi serikali ilivyoboresha mazingira ya kufanya biashara.

WABUNGE wameipogeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kufanikisha ujenzi na ukarabati wa soko la Kariakoo ambalo limeboreshwa na kuwa na viwango vya kimataifa.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Justin Nyamoga leo (Aprili 12,2025) Dar es Salaam wakati walipokagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo na maandalizi ya kuwarejesha wafanyabiashara.

“Sisi kama Bunge tumekagua na kujionea kazi kubwa ya Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan aliyetoa shilingi Bilioni 28.03 ili kujenga soko jipya na kukarabati lile lililoungua ambapo mradi huu utanufaisha watu wengi” alisema Nyamoga.

Nyamoga aliongeza kusema Wabunge wameridhishwa na viwango vya ubora na usalama vilivyowekwa katika Soko la Kariakoo unaolifanya kuwa na taswira ya kimataifa.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Festo Dugange alisema mradi huo ulianza kutekelezwa mwaka 2022 umefikia asilimia 98 ukigharimu zaidi ya Bilioni 28 ambapo utaongeza nafasi za biashara toka 1,662 hadi 1,907.

Dugange alieleza kuwa lengo la Serikali ni kuweka mazingira bora ya ufanyaji biashara katika soko la Kariakoo ambalo litafanya kazi kwa muda wa saa 24 kuwa maandalizi yamekamilika.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila alisema soko litafunguliwa hivi karibuni na kwamba Serikali itahakikisha wafanyabiashara wote wenye sifa wanapatiwa maeneo kulingana na sifa zilizoanishwa.

Akitoa taarifa kuhusu maandalizi ya kuwarejesha wafanyabiashara sokoni hapo, Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo CPA Ashraph Yusuph Abdulkarim alisema tayari wafanyabiashara 1,002 kati 1,520 wa kundi la kwanza wamepangiwa maeneo ndani na mfumo wa TAUSI.

CPA Abdulkarim aliongeza kusema, wafanyabiashara 518 kati ya 1,520 wana changamoto mbalimbali ikiwemo 194 kuwa na madeni ya nyuma, 134 hawajaza fomu maalum na 190 hawana namba ya kitambulisho cha Taifa (NIDA) na Namba ya Mlipa Kodi (TIN) , hivyo hawajapangiwa maeneo hadi sasa.

Halotel+Mpango+Mzima

No comments:

Post a Comment

Contact Form

Name

Email *

Message *

Contact Form

Name

Email *

Message *