|
Hafla ya Benki ya NMB kusaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na Shirika la
Korea Kusini linalojihusisha na kufadhili miradi katika sekta ya ujenzi la
Korea Finance for Construction (K-FINCO) kusaidia kuwawezesha wakandarasi wa
Korea Kusini kushiriki kikamilifu katika miradi ya ujenzi nchini Tanzania, ambapo
NMB itaiwakilisha K-FINCO kwa kutoa dhamana za kupata zabuni za kutekeleza
miradi hiyo. |
|
Hafla ya Benki ya NMB kusaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na Shirika la
Korea Kusini linalojihusisha na kufadhili miradi katika sekta ya ujenzi la
Korea Finance for Construction (K-FINCO) kusaidia kuwawezesha wakandarasi wa
Korea Kusini kushiriki kikamilifu katika miradi ya ujenzi nchini Tanzania, ambapo
NMB itaiwakilisha K-FINCO kwa kutoa dhamana za kupata zabuni za kutekeleza
miradi hiyo. |
|
Viongozi mbalimbali wa pande mbili wakiwa katika hafla ya Benki ya NMB kusaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na Shirika la
Korea Kusini linalojihusisha na kufadhili miradi katika sekta ya ujenzi la
Korea Finance for Construction (K-FINCO). |
|
Hafla ya Benki ya NMB kusaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na Shirika la
Korea Kusini linalojihusisha na kufadhili miradi katika sekta ya ujenzi la
Korea Finance for Construction (K-FINCO) kusaidia kuwawezesha wakandarasi wa
Korea Kusini kushiriki kikamilifu katika miradi ya ujenzi nchini Tanzania, ambapo
NMB itaiwakilisha K-FINCO kwa kutoa dhamana za kupata zabuni za kutekeleza
miradi hiyo. |
|
Hafla ya Benki ya NMB kusaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na Shirika la
Korea Kusini linalojihusisha na kufadhili miradi katika sekta ya ujenzi la
Korea Finance for Construction (K-FINCO) kusaidia kuwawezesha wakandarasi wa
Korea Kusini kushiriki kikamilifu katika miradi ya ujenzi nchini Tanzania, ambapo
NMB itaiwakilisha K-FINCO kwa kutoa dhamana za kupata zabuni za kutekeleza
miradi hiyo. |
BENKI ya NMB imesaini Mkataba wa Makubaliano (MoU) ya kushirikiana na Shirika la Korea Kusini linalojihusisha na kufadhili miradi katika sekta ya ujenzi la Korea Finance for Construction (K-FINCO).
Lengo la makubaliano hayo ni kusaidia kuwawezesha wakandarasi wa Korea Kusini kushiriki kikamilifu katika miradi ya ujenzi nchini Tanzania ambapo NMB itaiwakilisha K-FINCO kwa kutoa dhamana za kupata zabuni za kutekeleza miradi hiyo. Kwa mujibu wa makubaliano hayo, Benki ya NMB na K-FINCO zitakuwa na jukumu muhimu la kuvutia miradi mikubwa ya ujenzi itakayosaidia kuboresha maisha ya Watanzania. Ushirikiano huu pia unatarajiwa kuendeleza ukuaji wa mitaji, kutengeneza ajira, na kuifanya Tanzania kuwa kinara wa miundombinu katika ukanda huu.
Hafla ya utiaji saini ya ushirikiano huo imeshuhudiwa na Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Mheshimiwa Togolani Mavura. Ujumbe wa NMB uliongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu (CEO), Bi Ruth Zaipuna, huku ujumbe wa K-FINCO ukiongozwa na Dkt. Eunjae Lee, ambaye ni CEO wa taasisi hiyo na mwenyekiti wa bodi yake ya wakurugenzi.
Mkataba huo, ambao unatarajiwa kuimarisha maendeleo ya sekta ya ujenzi nchini, unazichagiza taasisi hizo mbili kufanya kazi kwa karibu zaidi ili kuchangia kikamilifu ukuaji wa uchumi wa Tanzania na jitihada za ujenzi wa Taifa.
Tunaimani kuwa hatua hii itaimarisha mahusiano ya kiuchumi na kidiplomasia kati ya Tanzania na Korea Kusini, na kukuza urafiki kati ya wananchi wa mataifa haya mawili.
No comments:
Post a Comment