RAIS WA UMOJA WA MABUNGE DUNIANI (IPU), SPIKA DKT. TULIA AKIMKABIDHI RAIS WA CLUB DE MADRID, ZAWADI KUTOKA IPU - THE HABARII

THE HABARII

HABARI | MATUKIO | MICHEZO.


ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday, 10 February 2024

RAIS WA UMOJA WA MABUNGE DUNIANI (IPU), SPIKA DKT. TULIA AKIMKABIDHI RAIS WA CLUB DE MADRID, ZAWADI KUTOKA IPU

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akimkabidhi Rais wa Club de Madrid, Mhe. Danilo Turk, zawadi ya ngao kutoka IPU katika Ofisi ndogo za IPU zilizopo New York nchini Marekani tarehe 8 Februari, 2024.


 
Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akisaini Kitabu cha Maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Namibia Mhe. Hage Geingob, katika Ofisi za Ubalozi wa nchi hiyo uliopo New York nchini Marekani leo tarehe 9 Februari, 2024. Mhe. Geingob alifariki dunia tarehe 4 Februari, 2024 katika Hospitali ya Lay Pohamba Jijini Windhoek alikokuwa anapatiwa matibabu ya saratani.


No comments:

Post a Comment