KILOMITA 603 ZA BARABARA ZAENDELEA KUJENGWA NCHINI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Tuesday 11 April 2023

KILOMITA 603 ZA BARABARA ZAENDELEA KUJENGWA NCHINI

Meneja wa Mradi wa BRT, Eng. Barakaeli Mmari akifafanua jambo kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila alipokagua maendeleo ya Ujenzi wa Mradi wa BRT III, kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Gongolamboto ambao ujenzi wake unaendelea.

Meneja wa Mradi wa BRT, Eng. Barakaeli Mmari akifafanua jambo kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila alipokagua maendeleo ya Ujenzi wa Mradi wa BRT III, kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Gongolamboto ambao ujenzi wake unaendelea.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila akizungumza na wanahabari mara baada ya kukagua Mradi wa BRT III, kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Gongolamboto ambao ujenzi wake unaendelea.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila akitoa maelekezo kwa Meneja wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka BRT, Eng. Barakaeli Mmari alipokagua Mradi wa BRT III, kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Gongolamboto ambao ujenzi wake unaendelea.

Muonekano wa moja ya kituo cha mabasi yaendayo haraka eneo la TAZARA ambacho ujenzi wake unaendelea.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila akizungumza na wanahabari mara baada ya kukagua Mradi wa BRT III, kutoka katikati ya jiji la Dar es Salaam hadi Gongolamboto ambao ujenzi wake unaendelea.

IMEELEZWA takriban miradi 16 ya ujenzi wa barabara yenye gharama ya shilingi trillion 1.4, sawa na kilomita 603 inaendelea kujengwa katika maeneo mbalimbali nchini katika kuhakikisha shughuli za kiuchumi na kijamii zinaendelea kuimarika na kuleta tija kwa wananchi.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila amesema hayo leo wakati akikagua maendeleo mradi wa barabara ya Mabasi yaendayo Haraka BRT III jijini Dar es Salaam.

Eng. Mativila ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na Barabara ya Mianzini-Olemringaringa-Sambasha KM 18, Ntendo-Muze-Kilyamatundu KM 179, na Malagarasi-Ilunde-Uvinza KM 51.1.

Mingine ni Barabara ya Karatu-Mbulu-Hydom-Sibiti-Lalago-Maswa KM 389, Matai-Kasesya KM 50, Ntyuka-Mvuni KM 76 na barabara ya Tarime-Mugumu KM 87.14.

Eng. Mativila amesema Serikali inatambua umuhimu wa barabara za lami na madaraja ya kisasa katika kuhakikisha barabara zinapitika wakati wote na hivyo kuleta tija katika shughuli za kiuchumi na kijamii kwa ujumla.

"Nawahakikishia wakazi wa Dar es salaam Barabara ya BRT II, na BRT III zitakamilika kwa mujibu wa mpango tuliouweka ili kupunguza changamoto ya msongamano wa magari katikati jijini la Dar es Salaam," amesisitiza Eng. Mativila.

Aidha amewataka mameneja wa TANROADS nchini kote kuhakikisha barabara zinapendezeshwa na kuwa katika hali bora wakati wote.

Kwa upande wake Meneja wa barabara za BRT Eng. Barakaeli Mmari amesema wamejipanga kuhakikisha magari yanaongozwa vizuri katika barabara zinazojengwa ili kupunguza msongamano wa magari na kuepuka ajali.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO TANROADS

No comments:

Post a Comment