WAZIRI WA UCHUMI WA FINLAND AWASILI TANZANIA KIKAZI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Sunday 29 January 2023

WAZIRI WA UCHUMI WA FINLAND AWASILI TANZANIA KIKAZI

 

Waziri wa Masuala ya Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Tapani Lintilä akimsikilza Balozi wa Finland Nchini, Mhe. Zitting Maria Theresa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

WAZIRI wa Masuala ya Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Tapani Lintilä amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 29 Januari hadi tarehe 1 Februari 2023. 

Lengo la ziara hiyo ni kujadili masuala yenye maslahi kwa Tanzania na Finland ili kuimarisha ushirikiano wa pande mbili kupitia Programu ya sasa ya Ushirikiano wa Maendeleo na biashara na kukuza ushirikiano wa kibiashara katika sekta ya biashara na uwekezaji.

Mhe. Lintilă akiwa nchini anatarajia kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe, Dkt. Stergomena Tax, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Pindi Chana, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf F. Mkenda.

Viongozi wengine ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe,  Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC); Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Shirika la Umerne Tanzania (TANESCO).

No comments:

Post a Comment