BENKI
ya NMB imeingia makubaliano na Mamlaka ya Hifadhi Mji Mkongwe, chini ya
usimamizi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale ya Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar kuboresha bustani ya Forodhani.
Chini
ya makubaliano hayo, Benki ya NMB itasimamia vipengele vifuatavyo:-
✅ Kuhakikisha uwepo wa
huduma na suluhishi za kifedha, elimu za kifedha na mikopo kwa wafanyabiashara
wa Forodhani.
✅ Kuweka maeneo maalum
ya polisi, kubadilishia nguo wapiga mbizi na NMB Wakala.
✅ Kuboresha maeneo ya
kupiga mbizi Forodhani, na kutoa maboya kwa wapigambizi kwa ajili ya usalama
wao.
✅ Kuboresha taa
zilizopo eneo la Forodhani
Makubaliano
haya yametiwa saini na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hifadhi Mji Mkongwe, Eng. Ali
Said na Afisa Mkuu wetu wa Wateja Binafsi na Biashara - Filbert Mponzi huku wakishuhudiwa na Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Mhe. Simai Mohamed Said na
viongozi wengine.
No comments:
Post a Comment