TAMASHA LA MSIMU LA UTAMADUNI LA AFRIKA KUSINI NA TANZANIA - THE HABARII

THE HABARII

HABARI | MATUKIO | MICHEZO.


ASAS GROUP

Habari Mpya


Saturday, 19 November 2022

TAMASHA LA MSIMU LA UTAMADUNI LA AFRIKA KUSINI NA TANZANIA

Naibu Waziri wa Utamaduni wa Afrika Kusini, Mhe. Mcawe Mafu akiongea na umati wa watanzania na Afrika Kusini wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Msimu wa Utamaduni wa Afrika Kusini na Tanzania ambalo linafanyika nchini kuanzia Novemba 18 hadi Desemba 04, 2022 na kusisitiza kuwa nchi hizo mbili ni ndugu wa muda mrefu.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Saidi Yakubu akisisitiza jamabo wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Msimu wa Utamaduni wa Afrika Kusini na Tanzania linalofanyika Novemba 18, 2022 katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Na Shamimu Nyaki

WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa amezindua Tamasha la Msimu wa Utamaduni wa Afrika Kusini na Tanzania linalofanyika nchini na kusisitiza kuwa Tamasha hilo linaimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.

 

Mhe. Mchengerwa amezindua Tamasha hilo leo Novemba 18, 2022 katika Ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam ambapo amesema Tanzania ni nchi pekee Afrika iliyohakikisha nchi nyingine za Bara hilo zinakua huru.

 

"Tanzania ndio nchi pekee yenye historia ya uhifadhi wa Ukombozi wa Bara la Afrika, vijana wanapaswa kutambua kuwa Taifa letu lilitoa machozi, jasho na damu kuhakikisha Afrika Kusini na Mataifa mengine ya Afrika yanakua huru", alisema Mhe. Mchengerwa.

 

Ameongeza kuwa, Tamasha hilo litaimarisha undugu wa nchi hizo na kukuza Sekta za Utamaduni na Sanaa ikiwa ni pamoja na kutangaza Utalii, Mila na Desturi za nchi hizo, ambapo amesisitiza wadau wa sekta hizo kujitokeza kuuza na kuonesha bidhaa zao katika msimu wa Tamasha hilo.

 

Amesema  Serikali ya Awamu ya Sita  chini ya Rais, Mhe. Samia  imeendelea kuboresha sekta hizo ambazo zimeajiri vijana wengi, huku akitoa wito kwa Sekta Binafsi kuunga mkono juhudi hizo.

 

Aidha, Mhe. Mchengerwa ametoa wito kwa Idara ya Utamaduni kuhakikisha inaandaa matamasha yenye sura ya kimataifa ambayo yatahusisha nchi nyingi zaidi.

 

Awali, Naibu Waziri wa Utamaduni wa Afrika Kusini, Mhe. Mcawe Mafu alisema nchi yake imeleta Tamasha hilo limeletewa Tanzania kwa kuwa nchi hizo ni ndugu wa muda mrefu.

 

Amesema Tamasha hilo litahusisha Sanaa za maonesho, mila na desturi, ngoma za asili pamoja na Semina kuhusu historia ya nchi hizo.


No comments:

Post a Comment