BARABARA YA KIMARA –KIBAHA NJIA NANE KUKAMILIKA OKTOBA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday, 10 August 2022

BARABARA YA KIMARA –KIBAHA NJIA NANE KUKAMILIKA OKTOBA

Muonekano wa Barabara ya Kimara – Kibaha (Km 19.2), ambao ujenzi wake kwa njia nane ukiwa unaendelea jijini Dar es Salaam.

Muonekano wa Daraja la Mbezi kwa Yusufu katika Barabara ya Kimara – Kibaha (Km 19.2), ambalo ujenzi wake unaendelea jijini Dar es Salaam.

Muonekano wa Barabara unganishi katika Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani cha Mbezi Lous (Stand ya Magufuli) ambayo ujenzi wake kwa kiwango cha lami unaendelea jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya akisisitiza jambo kwa wataalam wanaosimamia ujenzi wa Barabara ya Kimara – Kibaha (Km 19.2), ambao ujenzi wake unaendelea jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya akisisitiza jambo kwa wataalam wanaosimamia ujenzi wa Barabara ya Kimara – Kibaha (Km 19.2), ambao ujenzi wake unaendelea jijini Dar es Salaam.

Muonekano wa Daraja la Mbezi kwa Yusufu katika Barabara ya Kimara – Kibaha (Km 19.2), ambalo ujenzi wake unaendelea jijini Dar es Salaam.

NAIBU Waziri wa Ujenzi, Eng. Godfrey Kasekenya amemtaka Mkandarasi anayejenga Barabara ya Kimara – Kibaha (Km 19.2), pamoja na Barabara za maingilio katika Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo mikoani Mbezi-Magufuli kuhakikisha ujenzi huo unakamilika ifikapo Oktoba mwaka huu.

Akizungumza na wanahabari mara baada ya kukagua barabara hiyo leo jijini Dar es Salaam, Eng. Kasekenya amesema Serikali imeridhishwa na uboreshaji wa barabara za maingilio na madaraja katika eneo la mbezi hivyo kumtaka mkandarasi kumaliza kazi hiyo haraka iwezekanavyo na kwa ubora.

Amebainisha kuwa katika mkakati wa kupunguza msongamano jijini Dar es salaam tayari maandalizi ya kujenga kwa njia nane sehemu ya Kimara hadi Ubungo yameanza ili kuhakikisha hakuna msongamano wa magari kati ya  Ubungo-Kibaha.

 “..Asilimia themanini na nane iliyofikia inatosha kukamilisha kazi zilizobaki katika kipindi cha miezi miwili ijayo, hivyo TANROADS na Mkandarasi ESTIM hakikisheni kazi hiyo inakamilika kwa ubora,” alisisitiza Eng. Kasekenya.

Aidha amewaonya wezi wa miundombinu ya taa za barabara kuacha kufanya hivyo mara moja kwani usalama wa barabara ni pamoja na uwepo wa taa hizo, na kusisitiza umuhimu wa wananchi kutumia madaraja ya juu na kuvuka katika maeneo yaliyotengwa ili kupunguza ajali.

Naye Mhandisi Mkazi anayesimamia ujenzi wa Barabara hiyo, Injinia Mwanaisha Rajabu amemhakikishia Naibu Waziri Kasekenya kuwa atahakikisha barabara hiyo inakamilika kwa wakati na ubora uliokusudiwa ifikapo Oktoba.

 Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.

No comments:

Post a Comment