Naibu Waziri wa Ujenzi
na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya akipongezwa na kamati ya maandalizi ya
Bonanza la Sekta ya Uchukuzi baada ya kuzinduwa rasmi bonanza hilo. |
Naibu Waziri wa Ujenzi
na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya katika picha ya pamoja na Kamati ya
maandalizi ya Bonanza la Sekta ya Uchukuzi baada ya kulizinduwa rasmi bonanza
hilo. |
NAIBU Waziri wa
Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya ameipongeza sekta ya Uchukuzi
kwa kukuza vipaji katika michezo na hivyo kuiletea heshima Wizara ya Ujenzi na
Uchukuzi katika mashindano ya kitaifa.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam mara baada ya kuzindua Bonanza la Sekta ya Uchukuzi, Naibu Kasekenya amesema michezo licha ya kuburudisha na kuwaweka watu karibu hujenga afya ya mwili na akili na hivyo kuleta tija mahali pa kazi.
"Nawataka
wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kutenga bajeti ya
kutosha kwa ajili ya kuendeleza michezo na kuibua vipaji miongoni mwa watumishi
ili kuwawezesha kuwa wenye afya njema na kufanyakazi kwa bidii," amesema
Mhandisi Kasekenya.
Aidha
ameitaka kamati ya maandalizi kuhakikisha Bonanza la Tano linafanyikia mjini Dodoma ili kuongeza
idadi ya washiriki.
Naye
Mwenyekiti wa maandalizi ya bonanza hilo, Bw. Alphonce Mwingira amesema uwepo
wa tamasha hilo ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Ujenzi na
Uchukuzi, Dk. Leonard Chamuriho, kuhusu umuhimu wa michezo mahali pa kazi ili
kujenga umoja na ushirikiano.
Mbali na
michezo na burudani, katika bonanza hilo washiriki pia walipata fursa ya kupima
afya zao na kupata ushauri wa kitabibu.
Zaidi ya
taasisi 14 za sekta ya Uchukuzi, zikiwemo TAA, TMA, TCAA, LATRA, TASAC, TAZARA,
TRC, TPA, KADCO, ATCL, MSCL, SINOTASHIP, NIT na DMI zimeshiriki bonanza hilo
lilokuwa na michezo mbalimbali, ikiwemo mpira wa miguu, pete, kuvuta kamba,
mpira wa wavu, kucheza bao na riadha.
Imetolewa na Kitengo cha
Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.
No comments:
Post a Comment