WAZIRI KAMWELWE AWATAKA TEMESA KUJIPANGA - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Tuesday 20 October 2020

WAZIRI KAMWELWE AWATAKA TEMESA KUJIPANGA

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akibonyeza kitufe na kufungua pazia kuashiria uzinduzi rasmi wa kivuko kipya cha MV. UKARA II HAPA KAZI TU katika hafla iliofanyika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza. Kivuko cha MV. UKARA kimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 4.2 na kina uwezo wa kubeba abiria 300 na magari 10 sawa na tani 300.



Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kivuko kipya cha MV. UKARA II HAPA KAZI TU katika sherehe zilizofanyika katika Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza. Kivuko cha MV. UKARA kimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 4.2 na kina uwezo wa kubeba abiria 300 na magari 10 sawa na tani 300.


Wananchi wa visiwa vya Ukara, Bugorola na maeneo ya jirani wakisubiri kuingia katika kivuko kipya cha MV. UKARA II HAPA KAZI TU mara baada ya kuzinduliwa rasmi na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe katika sherehe zilizofanyika katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe akishuka kwenye kivuko kipya cha MV. UKARA II HAPA KAZI TU mara baada ya kukizindua rasmi mapema katika sherehe zilizofanyika katika kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza. 

Wananchi wakishangilia Kivuko kipya cha MV. UKARA ambacho kimejengwa na Serikali kwa gharama ya shilingi bilioni 4.2 na kina uwezo wa kubeba abiria 300 na magari 10 sawa na tani 300.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe,Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Malima, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Maselle, Katibu Mkuu wa Ujenzi Arch. Elius Mwakalinga, viongozi wa dini mbalimbali na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wa mkoa wa Mwanza wakiwaombea marehemu wa ajali ya kivuko cha MV. NYERERE kilichozama mwaka 2018 katika mnara wa kumbukumbu ilipozikwa miili ya baadhi ya wahanga wa ajali hiyo.

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Isack Kamwelwe ameutaka Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA), kuhakikisha huduma ya uendeshaji wa vivuko inakuwa salama na ya uhakika wakati wote.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kivuko kipya cha Mv. UKARA II kitakacho toa huduma kati ya Kisiwa cha Ukara na Bogorora wilayani Ukerewe, Eng. Kamwele amewataka Temesa kuwa wabunifu, wazalendo na wanaojifunza kila mara ili kuepuka kero na ajali zinazoepukika.

"Hakikisheni abiria na mizigo inayopakizwa kwenye kivuko inazingatia uwezo ili kulinda usalama wa abiria na mali zao", alisisitiza Waziri, Eng. Kamwelwe.

Ameongeza kuwa upo umuhimu wa Shirika la Wakala wa Meli, TASAC kukagua na kutoa elimu ya kutosha kwa wadau wote wa usafiri majini ili kuufanya usafiri huo kuwa salama wakati wote.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano sekta ya Ujenzi Arch. Elius Mwakalinga amesema Wizara itafunga mtambo wa Tehama utakaowezesha vivuko vyote nchini kufuatiliwa vinavyofanya kazi kwa kutokea Wizarani ili kupunguza changamoto zinazosababishwa na binadamu.

"Tumejipanga kuboresha usafiri kayika maziwa na bahari ili kuongeza fursa za ajira na uchumi kwa watanzania," amesisitiza Arch. Mwakalinga.

Aidha Katibu Mkuu huyo amempongeza mkandarasi Songoro Marine kwa kujenga kivuko hicho kipya na chakisasa kwa muda mfupi. Mtendaji mkuu wa Temesa Eng. Japhet Masele kilichogharimu shilingi bilioni 4.2 kina uwezo wa kubeba tani mia moja ikiwa ni abiria 300 na magari 10 kwa wakati mmoja.

Zaidi ya shilingi Bilioni 36.3 zimetumika katika ujenzi wa vivuko saba ambavyo ni Mv Ilemela, Mv, Mwanza, Mv Ukara II, Mv. Tanga, Mv. Kazi, Mv Chato na Mv. Mafia ambavyo kwa pamoja vitahuisha huduma za usafiri katika baadhi ya maeneo ya ziwa Victoria na Pwani ya Bahari ya Hindi.

Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano Serikalini Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. 

No comments:

Post a Comment