MBUNGE WA USHETU AHAMASISHA ELIMU NA MICHEZO JIMBONI KWAKE - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 2 October 2019

MBUNGE WA USHETU AHAMASISHA ELIMU NA MICHEZO JIMBONI KWAKE

Mbunge wa Ushetu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), Mhe. Elius John Kwandikwa akimkabidhi jezi nahodha wa timu ya waendesha bodaboda wa Kata ya Chambo baada ya timu hiyo kuifunga timu ya Itumbili bao 1-0 katika pambano la kuhamasisha umakini katika uendeshaji bodaboda jimboni Ushetu.

Mbunge wa Ushetu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), Mhe. Elius John Kwandikwa akisisitiza umuhimu wa waendesha bodaboda kujielimisha kuhusu usalama barabarani kabla ya kuanza kwa pambano la soka baina ya timu za Bodaboda na Itumbili katika jimbo la Ushetu. 

Mbunge wa Ushetu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), Mhe. Elius John Kwandikwa akisisitiza umuhimu wa wanafunzi kuhudhuria masomo katika Shule ya Msingi Mapamba katika jimbo lake.

Wanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Mapamba wakimsikiliza Mbunge wao ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), Mhe. Elius John Kwandikwa aliposisitiza umuhimu wa wanafunzi hao kuhudhuria masomo na kujifunza kwa bidii ili kuinua ufaulu jimboni humo.

Mbunge wa Ushetu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), mhe. Elius John Kwandikwa akimkabidhi cheti cha ufaulu mafunzo ya uendesha bodaboda mmoja wa waendesha bodaboda katika jimbo la Ushetu.

Mbunge wa Ushetu ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (sekta ya ujenzi), Mhe. Elius John Kwandikwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu za Bodaboda na Itumbili kabla ya kuanza kwa pambano la soka baina ya timu hizo.

No comments:

Post a Comment