MATAWI YA BENKI YA NMB KUHUDUMIA WATEJA HADI SAA MOJA JIONI - THE HABARII

ASAS GROUP

Habari Mpya


Wednesday 2 October 2019

MATAWI YA BENKI YA NMB KUHUDUMIA WATEJA HADI SAA MOJA JIONI

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bi. Siporah Liana (kulia) pamoja na Ofisa Mkuu wa Fedha Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna wakikata keki kuashiria uzinduzi wa maadhimisho ya  Wiki ya Huduma kwa Wateja Benki ya NMB leo jijini Dar es Salaam. 


Ofisa Mkuu wa Fedha Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna (kushoto) akimlisha keki mgeni rasmi Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bi. Siporah Liana (kulia) kwenye hafla ya uzinduzi wa maadhimisho ya  Wiki ya Huduma kwa Wateja Benki ya NMB leo jijini Dar es Salaam. 

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bi. Siporah Liana (kulia) akizungumza kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja Benki ya NMB leo jijini Dar es Salaam. 

Ofisa Mkuu wa Fedha Benki ya NMB, Ruth Zaipuna akizungumza na wateja (hawapo pichani) kwenye uzinduzi wa maadhimisho Wiki ya Huduma kwa Wateja jijini Dar es Salaam. 

Mmoja wa wateja wa Benki ya NMB Tawi la Mlimani City akitoa shukrani kwa benki hiyo kwenye uzinduzi wa maadhimisho Wiki ya Huduma kwa Wateja jijini Dar es Salaam. 
  
Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Mlimani City, Irine Masack akiitambulisha timu inayowahudumia wateja katika tawi hilo.

Baadhi ya wateja wakiwa katika hafla hiyo iliyofanyika Tawi la NMB, Mlimani City jijini Dar es Salaam.

BENKI ya NMB imeongeza muda wa kufanya kazi kwa baadhi ya matawi yake ikiwa ni sehemu ya maboresho ili kuhakikisha wateja wake wanapata huduma kwa ufasaha. Kwa kuanzia mwezi huu matawi ya NMB Kongo, NMB Mlimani City na Kahama Business Centre yatafanya kazi hadi saa moja jioni.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa maadhimisho Wiki ya Huduma kwa Wateja, Ofisa Mkuu wa Fedha Benki ya NMB, Ruth Zaipuna amesema kuanzia mwezi Oktoba matawi yaliotajwa yatakuwa yanafunguliwa saa nne asubuhi na kufungwa saa moja jioni.

Mbali na mabadiliko hayo, NMB pia imeongeza muda wa kuhudumia wateja kwa kitengo chetu cha Huduma kwa Wateja, badala ya kufunga saa nne usiku, kuanzia mwezi huu kituo hicho kitakuwa kinafungwa saa sita kamili usiku.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Bi. Siporah Liana aliipongeza NMB Benki kwa maboresho inayoyafanya kwani yanazidi kuwavutia wateja wengi. Aliipongeza benki hiyo kwa huduma za kijamii ambazo imekuwa ikijitoa katika nyanja za elimu, afya na majanga mengine yanayojitokeza kwa jamii yetu.

"...Mnafanya mambo makubwa kwa jamii, nimeona kuna sehemu unajitolea madawati na viti kwa shule, vifaa tiba katika hospitali na vituo vya afya na mnasaidia kwenye majanga tunawahakikishia mchango wenu unaonekana kwa jamii endeleeni kuisaidia," alisema Bi. Siporah Liana.

Awali akizungumza, Bi. Zaipuna alibainisha kuwa kwa sasa huduma za NMB zipo kwa kila wilaya huku ikijivunia kutoa huduma nafuu zaidi. "...Mpaka sasa tuna matawi 230, ATM Zaidi ya 800 na NMB Wakala Zaidi ya 6000. Ndugu Mgeni Rasmi, maboresho haya yote situ kwaajili ya mwezi huu wa huduma kwa wateja, bali ni endelevu." Alisema ofisa huyo mwandamizi wa NMB.

Mwezi wa 10 kila mwaka,dunia huadhimisha Wiki ya Huduma kwa Wateja. Kwa NMB siku hii tunaichukulia kama fursa muhimu ya kuendeleza maono ya benki – Kumjali Mteja katika matawi yetu yote.

No comments:

Post a Comment